Monday 24 July 2017

Makampuni yajitokeza kudhamini Kilifm Marathon

Mratibu wa mbio za Kilifm Marathon, Nelson Mrashani akizungumza kuhusu mbio hizo hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI zimezidi kujitokeza kufanikisha mbio za pili za Kilifm Marathon zitakazofanyika Agosti 13 mjini Moshi.

Mratibu wa mbio hizo Nelson Mrashani akizungumza kwa njia ya simu jana alisema maandalizi yanaenda vizuri na wamepata wadhamini.

Mrashani aliwataja wadhamini hao kuwa ni pamoja na Wiva Entertaiment, Mr UK, Maji ya Kilimanjaro, Kampuni ya Coca Cola, Radio Kilfm, Temeck Car Tracking, Tanzania Media Foundation, Finca Bank na Ciascom Tech Engeeniring.

Alisema kuwa tayari usajili wa mbio hizo umeanza, ambapo mwaka huu wanatarajia kupata washiriki zaidi ya 3,000 kutoka ndani na nje ya nchi.

Mbio hizo aitahusisha umbali wa kilometa 21, kilometa tano , ambazo zitawashirikisha wafanyakazi wa taasisi mbalimbali pamoja na watu wazima wakati zile za kilometa 2.5 zitakuwa na watoto wadogo.
Zawadi za washindi zitakuwa za aina tofauti, ambapo washiriki wa kilometa 21 wenye umri wa miaka 45-60 na hadi 100 watapewa zawadi maaluma wakati wakibiaji wakawaida watakuwa na kundi lao.

Pia washindi watatu watatu wa mbio zote watapata fursa ya kwenda kutembelea hifadhi ya Ngorongoro ili kuhamasisha utalii wa ndani kupitia Kituo cha Kilifm Sport Centre.

Mrashani alisema kuwa bado wanakaribisha wadhamini wengine ili kuzidi kuboresha mbio hizo ambazo zitakuwa za aina yake mwaka huu.

No comments:

Post a Comment