Saturday 15 July 2017

Ziara ya Waziri Mbarawa Kiwanja cha ndege JNIA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (kulia) akifurahia jambo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Phillip Mpango (kushoto)  na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba na Katibu Mkuu  sekta ya Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho (mwenye mkoba mweusi) leo walipokutana kwenye Jengo la Watu Mashuhuri la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Katibu Mkuu wa Chama cha Madereva wa Taxi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Simon Mwampashi (kulia), akitoa maoni mbalimbali kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa alipofanya ziara JNIA.
  1. Mkuu wa Kitengo cha Idara ya Uhamiaji Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Bw. Flugence Andrew (kulia) akitoa maelezo ya utaratibu unaotumika kulipia viza kwa Mhe. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano leo alipofanya ziara kwenye jengo la abiria la kiwanja hicho. 
Ofisa wa Benki ya NMB, Leah Rutayungurwa  (aliyendani ya dirisha) leo akimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof Makame Mbarawa aliyetaka kujua muda anaohudumiwa abiria mmoja wakati akilipia viza kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA).
Ofisa Forodha Msaidizi, Hezron Giso (kulia), akielezea shughuli anazozifanya ndani ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA), kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (mwenye miwani kifuani), wakati wa ziara ya Waziri iliyofanyika leo.
Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TBII-JNIA), mwenye kizibao akielezea jambo katika meza ya ukaguzi wa tiketi za abiria wanaosafiri. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA),  Salim Msangi.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akiwa katika mfumo wa kupokelea mizigo kwa abiria wanaowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere alipofanya ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali. Mwenye kizibao ni Kaimu Mkurugenzi wa kiwanja hicho, Joseph Nyahende.

No comments:

Post a Comment