Saturday 15 July 2017

Taifa Stars yajiweka pabaya Chan 2018 Nairobi



Na Mwandishi Wetu, Mwanza
KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Mayanga amesema kuwa timu yake imeshindwa kuibuka na ushindi katika mchezo wa kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (Chan) kwa wachezaji wa nyumbani baada ya kufungwa bao la mapema na Rwanda kwenye Uwanja wa CCM Kirumba hapa.

Taifa Stars ilifungwa bao katika dakika ya 17 na kuwa na kibarua cha kutafuta bao la kusawazisha, ambalo walilipata kwa penalti.

Mayanga aliyasema hayo baada ya mchezo huo was are ya kufungana bao 1-1 na timu yake kujiweka katika nafasingumu ya kusonga mbele katika mashindano hayo. Bao la wageni lilipachikwa na Dominique Nshuti.

Kukosa utulivu ni jambo jingine ambalo limechangia Taifa Stars kushindwa kupata matokeo ya ushindi. Mayanga alisema kuwa wapinzani wao walitumia mbinu ya kupoteza muda ili kupata matokeo ya sare.


Naye kocha wa Rwanda alisema kuwa wanajipanga kqa ajili ya mchezo wa marudiano kwani mchezo huo bado haujamalizika lakini alisema timu ya Tanzania sio timu ya kuibeza kwani iko vizuri.

Matokeo hayo yanamaanisha Taifa Stars italazimika kwenda kushinda ugenini mjini Kigali Julai 22 ili kusonga mbele katika kuwania tiketi ya CHAN mwakani nchini Kenya, ambako itamenyana na mshindi kati ya Sudan Kusini na Uganda zilizotoa sare ya 0-0 pia jana mjini Juba.

No comments:

Post a Comment