Sunday 24 April 2016

Wakenya watamba London Marathon 2016 baada ya kushika nafasi za kwanza kwa wanawake na wanaume



LONDON, Uingereza

WAKENYA leo wametamba katika mbio za London Marathon baada ya kushika nafasi ya kwanza kwa upande wa wanawake na wanaume.

Kwa upande wa mademu, Jemima Sumgong ameshinda mbio hizo licha ya kudondoka wakati akishindana katika shindano hilo.

Mwanariadha huyo (31) alianguka na kugonga kichwa chini baada ya kusukumwa na mwanariadha wa Ethiopia Aselefech Mergia wakati wakiwa wanakaribia katika sehemu ya maji.

Lakini licha ya dhahama hiyo bado mwanadada huyo alisimama na kuendelea kukimbia akiwa pamoja na kundi hilo la wanariadha wenzake.

Alionesha umakini mkubwa na kuwastaajabisha watu baada ya kuwashinda wanariadha hao na kisha kuchukua taji lake hilo la kwanza kwa kutumia muda wa saa 2 dakika 22 na sekunde 58.

Pia mwanariadha Tigist Tufa wa Ethiopia ambaye alikuwa bingwa wa mwaka 2015 aliibuka wa pili katika shindano hilo akiwa nyuma ya mshindi kwa sekunde tano tu.

Katika michuano hiyo bado Wakenya walionekana kutamba zaidi kwa kuwa hata mshindi wa tatu alitokea Kenya ambaye ni Florence Kiplagat.

Wakati huo huo, mwanariadha Eliud Kipchoge alishinda shindano la upande wa wanaume katika mbio hizo.

Mshindi huyo ameonekana kuweka rekodi ya aina yake kwa kuwa licha ya kuwa na umri mkubwa, lakini bado aliibuka mshindi.

Alitumia muda wa saa 2 dakika 3 na sekunde 5 kumaliza na kuibuka na ushindi huo ambapo akionekana akiwa amechoka.

No comments:

Post a Comment