Friday 1 April 2016

Ibrahimovic ataka sh. 1,881,000,000 kwa wiki kusajiliwa klabu za Ligi Kuu England



LONDON, England
MCHEZAJI Zlatan Ibrahimovic anataka apewe kiasi cha pauni 600,000 (sawa na sh. 1,881,000,000)kwa wiki ili kuchezea klabu ya Ligi Kuu ya England.

Kiasi hicho cha fedha kimebainishwa na mchezaji huyo ambaye ataondoka katika klabu yake ya sasa ya Paris Saint-Germain akiwa huru katika kipindi cha majira ya joto.

'Tunataka kumsajili, lakini kiasi cha fedha anachotaka alipwe ndio tatizo,' kilisema chanzo cha ndani. ‘Tukifanikiwa hilo tutakuwa tumefanya jambo kubwa sana kumpata, lakini ukweli anahitaji kiasi hicho cha fedha, akiwa na umri wa miaka 34?
Ibrahimovic amekuwa akifanya mazungumzo na timu za China, ambako inasakiwa kuwa ameahidiwa kupewa kiasi cha pauni milioni 1 kwa wiki endapo atatua huko, lakini hana mpango wa kuhamia Mashariki ya Mbali.

Badala yake ameziambia klabu za Uingereza kuongeza mshahara wake aliokuwa akiupta PSG, ambako aliwapeleka mabingwa hao wa Ufaransa kutwaa taji jingine.

Ibrahimovic yuko mbioni kwenda kucheza England lakini ikiwa na maana kuwa kolabu moja itakuwa inatoa mshahara mkubwa nchini. Anaamini kuwa hatakuwa na furaha kutokana na kodi zilizotozwa Uingereza.

Mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa katika Ligi Kuu ya England kwa sasa ni Wayne Rooney, ambaye anaondoka na kitita cha pauni 260,000.

Arsenal, Manchester United, Chelsea na hata West Ham zimekuwa zikihusishwa na mshambuliaji huyo wa Sweden.

Wakala wa Ibrahimovic Mino Raiola aliliambia gazeti la Dello Sport: 'Ukiiondoa Manchester City, ambayo itamchukua (Pep) Guardiola, klabu zote kubwa zimepiga hodi zikitaka kumchukua kocha huyo.
 
Mahitaji hayo makubwa anayotaka Ibrahimovic bila shaka yatazigharimu klabu angalau pauni milioni 31 kwa msimu mmoja tu katika mkataba wake huyo anaoutaka.

No comments:

Post a Comment