Saturday 9 April 2016

Uchukuzi Sports Club yajifua kwa mashindano ya Mei Mosi yatakayofanyika Dodoma


Timu ya soka ya Uchukuzi Sports Club ikifanya mazoezi wakijiandaa kwa mashindano ya Mei Mosi

Na Cosmas Mlekani
TIMU ya Uchukuzi Sports Club imetamba kufanya vizuri katika mashindano ya Mei Mosi yatakayofanyika mjini Dodoma kuanzia Aprili 16 mwaka huu.
Wachezaji wa Uchukuzi Sports Club wakijifua kwa ajili ya Mei Mosi.
Mwenyekiti wa timu hiyo inayoundwa na wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mohamed Ally alisema kuwa yake itafanya vizuri katika mashindano hayo.

Ally alisema kuwa kwa sasa wako katika mazoezi makali kujiandaa na mashindano hayo, ambayo yatafikia kilele chake Mei Mosi mjini Dodoma.

Akinana wa Uchukuzi wakijifua kwa ajili ya kuvuta kamba.
Alisema Uchukuzi Sports Club ina timu za soka, netiboli, kuvuta kamba, bao, karata, riadha, baiskeli na vishale.

Alisema kuwa wana uhakika timu yao kutamba katika mashindano hayo ya Mei Mosi kutokana na kufanya maandalizi kabambe chini ya makocha wa kimataifa na wazoefu.

Ally aliwataja baadhi ya makocha ho kuwa ni pamoja na Kenny Mwaisabula, Robert Damian, Terry, Kingsley Malwilo na Abunu Issa, ambao wameifanya timu yao ya soka kuwa tishio kwa timu zingine.

Alisema kuwa timu zao hizo zimekuwa zikicheza mechi kibao za majaribio ili kuwawezesha makocha kubaini makosa na kufanya marekebisho ya mwisho kabla timu hiyo haijaondoka kwenda Dodoma.

Naye Meneja wa Uchukuzi Sports Club, Damiani alisema kuwa timu yao inatarajia kwenda Dodoma Aprili 14 tayari kwa mashindano hayo.

Alisema timu ya soka na netiboli zimefanya majaribio kadhaa ili kujiweka fiti kwa mashindano hayo, ambayo wana uhakika wa kutwaa ubingwa.
Kikosi kabambe cha timu ya soka ya Uchukuzi kikiwa pamoja na kocha na meneja wa timu hiyo Robert Damiani (kushoto).

No comments:

Post a Comment