Tuesday 5 April 2016

Conte atua rasmi Chelsea, Sutton amponda asema hataleta miujiza



LONDON, England
UTEUZI wa Chelsea kumfanya Antonio Conte kuwa mbadala wa muda mrefu wa Jose Mourinho hakuna maana yoyote, anasema mshambuliaji wazamani wa Blues Chris Sutton.

Mourinho, 53, alitimuliwa Desemba nwaka jana akidaiwa kutoelewa na baadhi ya wachezaji wakubwa wa timu hiyo.

Conte, alitua jijini hapa na kumwaga wino wa kuifundisha timu hiyo kwa miaka mitatu baada ya kumalizika kwa msimu huu.

"Ikiwa atakuja hapa na kuanza kukorofishana na wachezaji, basi anaweza kukosa mafanikio, alisema Sutton.

Chini ya Mourinho, Chelsea ilitwaa taji la Ligi Kuu ya England ikiwa na point inane zaidi msimu uliopita na pia ilitwaa Kombe la Ligi.

Lakini timu hiyo ilipoteza mechi zake tisa kati ya 16 za mwanzo za ligi na walikuwa katika nafasi ya 16 katika msimamo, pointi moja juu ya ukanda wa kushuka daraja, wakati Mourinho akitimuliwa.

Kocha wazamani wa Uholanzi Guus Hiddink, aliyeteuliwa kuchukua kwa muda nafasi ya Mourinho hadi mwishoni mwa msimu, hajapoteza mchezo wowote kati ya 15 tangu achukue timu hiyo.

Hatahivyo, the Blues imemchukua Conte, ambatye atawasili katika klabu hiyo mara baada ya kumalizika kwa fainali za Mataifa ya Ulaya za  Euro 2016 kama kocha wao wa kudumu.

"Chelsea walikuwa na nafasi nzuri ya kumbakisha Hiddink," aliongeza Sutton,mwenye umri wa miaka 43. Na chini yake timu iliimarika kila mahali.

Conte alishinda taji la Serie A katika miaka yake mitatu wakati akiwa kocha wa Juventus, kabla hajaachia ngazi na kutua katika timu ya taifa ya Italia mwaka 2014.

Wachezaji wazamani wa Chelsea Andy Townsend na Pat Nevin wote wanaamini the Blues imefanya uteuzi mzuri
 .
"Sifikiri kama Conte atafanya tofauti na vile ambavyo alikuwa akipenda Jose katika kiwango chake, alisema kiungo wazamani wa kimataifa wa Ireland Townsend.

Moja ya kazi ya Conte atakapotua Stamford Bridge inaweza kuwa ni kufanya uamuzi wa mwisho kuhusu hatma ya John Terry.

Nahodha huyo wa Chelsea mwenye umri wa miaka 35 atamaliza mkataba wake katika kipindi cha majira ya joto na anasema bado hajapewa mkataba mpya.

Lakini Townsend anaamini kuwa kuwasili kwa Conte kunaweza kusaidia kuongeza mkataba kwa beki huyo wazamani wa England ili aweze kuendelea kubaki Stamford Bridge.

Conte pamoja na kujihakikishia kibarua Chelsea, lakini hajaahidiwa fungu na mmiliki wa timu hiyo Roman Abramovich ili kusajili wachezaji wapya.

Lakini mshambuliaji huyo wazamani wa England anafikiri the Blues itapambana kuvutia wachezaji wa kubwa Ulaya bila kuvuruga sheria za matumizi ya fedha katika usajili.

Chelsea,ambayo ilitwaa taji la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya mwaka 2012 na lile la Ligi ya Ulaya mwaka 2013, wako katika nafasi ya 10 katika Ligi Kuu ya England, wakipitwa pointi 10 na timu nne za kwanza katika msimamo huo.

No comments:

Post a Comment