Wednesday 13 April 2016

Mwadui v Azam, Yanga na Coastal Union nusu fainali Kombe la Shirikisho

Na Mwandishi Wetu
RATIBA ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) imefanyika usiku wa jana, huku timu za Coastal Union na Mwadui FC zikipata nafasi ya kucheza nyumbani.

Katika droo hiyo iliyochezeshwa na mchezaji mstaafu wa timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars), Esther Chaburuma, vigogo wa Ligi Kuu ya Vodacom, Azam FC na Yanga wakipata nafasi ya kucheza michezo hiyo katika viwanja vya ugenini.

Mwadui FC watakua wenyeji wa Azam FC katika mchezo unaotarajiwa kucheza Aprili 24, 2016 mjini Shinyanga, huku Wagosi wa Kaya Coastal Union wakicheza dhidi ya Yanga katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga siku hiyo hiyo.

Washindi wa michezo hiyo ya Nusu Fainali, watakutana fainali ya kombe hilo itakayofanyika mwezi Mei, ambapo Bingwa wake ataiwakilisha Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC).

Wakati huohuo, wadhamini wa michuano hiyo Azamtv kupitia kituo chake cha michezo cha Azam Sports, walilionesha hadharani kwa mara ya kwanza kombe la ubingwa na kulikabidhi kwa Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine.

No comments:

Post a Comment