Saturday 30 April 2016

Manchester United yataka kuchelewesha ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa Leicester City Jumapili



Kikosi cha Manchester United.

MANCHESTER, England
KIKOSI cha Manchester United huenda kisibadilike kutoka kile kilichoshinda mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA wakati timu hiyo Jumapili itakapokutana na `bingwamteule wa Ligi Kuu Leicester.

Wachezaji kama Luke Shaw, Bastian Schweinsteiger na Will Keane wataendelea kubaki nje ya uwanjani katika pambano hilo la aina yake.

Leicester City wenyew watajaribu kutwaa taji hilo la Ligi Kuu bila ya kuwa na mshambuliaji wake hatari Jamie Vardy, anayetumikia nyongeza ya adhabu ya kufungiwa mechi moja zaidi kufuatia kutoa maneno makali wakati akitolewa nje na mwamuzi walipocheza dhidi ya West Ham.

Mchezaji aliyechukua nafasi yake walipocheza dhidi ya Swansea wiki iliyopita, Leonardo Ulloa, ataanza katika mchezo huo dhidi ya Man United baada ya kupona maumivu ya mgongo.

MAONI YA WACHAMBUZI

Guy Mowbray: "Nimetabiri kuwa katika mchezo huo Man United itaifunga Leicester City'.

"Ndio, wanaweza kuongeza mwishoni mwa mchezo.

"Kitu ambacho hatutakuwa na wasiwasi nacho ni kwamba Leicesterwatakuwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England, wakikumbushia Arsenal mwaka 2002 kwa kuthibitisha hilo kwenye uwanja huo, ambayo umewahi kuandaa sherehe nyingi za ubingwa mara nyingi kuliko mahali kwingine.

"Man United watataka kushinda mchezo huo kwenye Uwanja wa Old Trafford, ili waweze kumaliza angalau katika nafasi ya nne za juu.”

"Mei Mosi mi alama ya kuanza vizuri, mwanzo mpya…”

WANACHOSEMA MAKOCHA

Kocha wa Manchester United Louis van Gaal: "Nafikiri tunatakiwa kuwafunga kwa sababu bado tuko katika mbio za kusaka nafasi ya nne. Hatuwezi kukubali wawe mabingwa wikiendi hii kwenye uwanja wetu wa Old Trafford.

"Nafikiri wanaweza kuwa mabingwa baadae wiki ijayo. Hatuharibu sherehe yao, ila tunaiharisha tu kidogo.

Kocha wa Leicester City Claudio Ranieri: "Ni kitu kisichoaminika, ni historia na hilo tunalijua.

"Ni muhimu kumaliza historia kama sinema ya Kimarekani. Wakati wote mwishoni ni mzuri, umalizika vizuri.

"Ni nafasi nzuri lakini kwa sababu hii tunatakiwa kuangalia. Acha niw kimya, tusubiri, tuna muda bado.

"Niliwaambia, kila kitu kipo mikononi mwetu na lazima tuendelee. Watu wengine watafurahia hilo lakini mimi lazima kusonga mbele.

UTABIRI WA LAWRO

Mchezo huu sio lazima Leicester ishindi lakini kwa Manchester United, wanatakiwa kushinda kwa kuwa wanahitaji ushindi ili waendelee kubaki katika nne bora.

Nafikiri mchezo huo utamalizika kwa sare, ambayo itakuwa nzuri kwa Leicester, ingawa utachelewesha ubingwa wao hadi Jumatatu usiku wakati Tottenham watakapocheza na Chelsea.

No comments:

Post a Comment