Thursday 24 September 2015

Waziri Celina Kombani afariki dunia nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi), Celina Kombani (pichani), amefariki dunia jana akiwa nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu. 

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah na baadhi ya wabunge waliozungumza jana, walisema Waziri Kombani alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu. 

Kwa mujibu wa Katibu huyo wa Bunge, Kombani alikuwa akisumbuliwa na magonjwa hayo kwa muda mrefu na kwamba mwili wake utarejeshwa nchini kesho. 

Kashilillah alisema Bunge pamoja na Serikali kwa kushirikiana na familia ya marehemu wanafanya taratibu za mazishi.

Hadi kifo chake, Waziri Kombani alikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki mkoani Morogro kwa tiketi ya CCM na pia alikuwa ndiye mgombea wa chama hicho katika jimbo hilo kwa uchaguzi wa mwaka huu.

Pamoja na kuwa Waziri katika Ofisi ya Rais (Utumishi), Kombani aliwahi kutumikia wizara mbalimbali ikiwemo ya Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mkoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na pia Waziri wa Katiba na Sheria.

No comments:

Post a Comment