Thursday 24 September 2015

Arsenal kupepetana na Sheffield Wednesday raundi ya nne Kombe la Ligi england



LONDON, England
TIMU ya daraja la kwanza ya Sheffield Wednesday itaikaribisha Arsenal katika mchezo wa raundi ya nne wa michuano ya Kombe la Ligi baada ya kuifungisha virago Newcastle United  juzi.

Liverpool, ambayo ilihitaji penalti ili kuiondoa Carlisle, itakuwa nyumbani kucheza dhidi ya Bournemouth.

Manchester United itakuwa mwenyeji wa Middlesbrough, wakati Crystal Palace itasafiri kuifuata Manchester City.

Mabingwa watetezi Chelsea watakuwa wageni wa Stoke City, wakati Southampton ikipangwa na Aston Villa na Norwich City watacheza na Everton.

Hull City, moja kati ya timu tatu za daraja la kwanza zilizomo katika ratiba hiyo, watakuwa wataikaribisha Leicester, ambapo mechi zitachezwa Oktoba 27 na 28 mwaka huu.

Ratiba raundi ya nne Kombe la Ligi

Manchester City v Crystal Palace

Liverpool v Bournemouth

Manchester United v Middlesbrough

Everton v Norwich City

Southampton v Aston Villa

Sheffield Wednesday v Arsenal

Hull City v Leicester City

Stoke City v Chelsea

No comments:

Post a Comment