Saturday 12 September 2015

Serena Williams afungwa na kibonde na kutolewa mashindano ya US Open



NEW YORK, Marekani
MCHEZAJI tenisi nguli Serena Williams juzi alishindwa kutimiza ndoto yake ya kufanya vizuri zaidi katika mashindano makubwa ya tenisi baada ya kutolewa katika michuano ya US Open.

Williams, mwenye umri wa miaka 33, alijikuta akitupwa nje ya mashindano hayo na mchezaji asiye hata na viwango katika orodha ya wachezaji wa tenisi duniani Roberta Vinci wa Italia kwa seti 2-6 6-4 6-4.

Kipigo hicho kimemfanya Williams kushindwa kutinga fainali ya mashindano hayo itakayofanyika leo jijini hapa.
Roberta Vinci wa Italia ndiye aliyemfunga Serena Williams na kumtupa nje ya mashindano ya US Open kwa seti 2-6 6-4 6-4.
"Haya ni matokeo ya kushangaza zaidi katika historia ya mchezo wa tenisi duniani, kwa sababu aliyepewa nafasi kubwa ndiye aliyeondolewa.

Williams aliaunza mchezo huo wa Ijumaa wa nusu fainali akiwa ameshinda mechi 33 mfululizo za mashindano makubwa ikirejea nyuma ile ya Wimbledon 2014.
Mchezaji huyo alikuwa na matarajio ya kufikia rekodi ya Steffi Graf ya mwaka 1988 ya kutwaa mataji wanne makubwa katika mwaka mmoja, na aliuwa akicheza na mchezaji aliyemfunga mara nne bila ya kuambulia seti.

Vinci, 32, yuko katika namda 43 katika orodha ya ubora wa wachezaji na kwa mara ya kwanza alikuwa akicheza nusu fainali ya mashindano makubwa.

"Roberta Vinci, ni mcheaji mdogo, akiwa na rekodi ya kushindwa na sasa anaingia katika mashindano ya US Open," alingeza Austin.
"Nilishinda mashindano matatu makubwa mwaka huu, " alisema  Williams. "Ndio, kama ningeshinda mataji manne mfululizo ingewa jambo la faraja zaidi.

No comments:

Post a Comment