Thursday 24 September 2015

Mtu aliyegoma kuacha kuvuta sigara ndani ya ndege apigwa faini na kufunguliwa mashtaka





BRISBANE, Australia
MTU mmoja ambaye aligoma kuacha kuvuta sigara katika ndege kutoka Sydney kwenda Sunshine Coast alijikuta matatani na kupigwa faini ya dola za Marekani 850 ikiwa ni mara 10 ya gharama ya njia moja ya tiketi.

Polisi walisema kuwa mfanyakazi wa ndege alimuomba mtu huyo mwenye umri wa miaka 37 kuacha kuvuta sigara wakati wa safari hiyo ya ndege ambayo ingechukua dakika 90 jana, lakini alipuuza na kuendelea kupuliza moshi hewani.
 
Wakati ndege hiyo ilipotua katika uwanja wa ndege wa Sunshine Coast majira ya saa 12:30 jioni, polisi waliingia ndani ya ndege hiyo na kumkamata mtu huyo.

Mtu huyo kutoka Caboolture (Kaskazini ya Brisbane, Australia),kilometa 55 kusini mwa pwani ya Sunshine na kufunguliwa mashtaka na anatakiwa kufika mahakamani Oktoba 12, polisi ilisema.

Mapema mwaka huu, abiria aliyepanda ndege hiyo ya Jetstar kutoka Gold Coast kwenda Sydney aliwasha sigara katika chumba cha kupumzikia, na kulazimisha ndege kubadili mwelekeo na kwenda Newcastle ambako ilitua kwa dharura.

Kuvuta sigara kumepigwa marufuku ndani ya ndege za Australia na atakayepuuza amri hiyo anapigwa faini ya dola za Marekani850.

No comments:

Post a Comment