Saturday 26 September 2015

Man City yachapwa 4-1, Arsenal, Liverpool mambo saaafii


Mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling akikimbia na mpira walipocheza na Tottenham Hotspur kwenye Uwanja wa White Hart Lane leo. Man City ilifungwa mabao 4-1.

LONDON, England
HARRY Kane jana alimaliza ukame wa kutofunga kwa saa 13 baada ya leo kufunga bao wakati Tottenham ikitoa kichapo kikali cha mabao 4-1 kwa vinara Manchester City 4-1.

Hicho ni kipigo cha pili mfululizo kwa Man City katika mechi za Ligi Kuu  ya England.

Mshambuliaji huyo wa England alifanya matokeo kuwa 3-1 katika dakika 61 baada ya mkwaju wa adhabu wa Christian Eriksen ulipogonga mwamba na kurudi uwanjani, wakati Spurs ikitoka nyuma kufuatia bao la kwanza lililofungwa na Kevin De Bruyne.

De Bruyne kama alikuwa katika nafasi ya kuotea lakini aliweza kuifungia Man city bao katika dakika ya 25, na mwamuzi alishindwa tena kubaini mpira wa kuotea wakati Eric Dier akiwasawazishia wenyeji.

Lakini hakukuwa na tatizo kwa mpira wa kichwa uliopigwa na Toby Alderweireld na kujaa wavuni na kuifanya Spurs kuwa mbele kabla Erik Lamela hajamzunguka Willy Caballero na kuipatia timu yake bao la nne.

Nayo Arsenal leo ilibuka na ushindi mnono baada ya kuifunga Leicester na kuhitimisha timuhiyo kuanza ligi bila kufungwa katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa King Power.

Alexis Sanchez baada ya ukame wa kutofuga, hatimaye jana alifunga hat-trick na kuiwezesha timu hiyo kutoka kifua mbele na pointi zote tatu.

Arsenal ilitoka nyuma na kuibuka na ushindi huo huku mabao mengine yakifungwa na Theo Walcott na Olivier Giroud  aliyefunga akitokea baada ya kuingia uwanjani akitokea.

Wayne Rooney aliifungia Manchester United wakati ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sunderland kwenye Uwanja wa Old Trafford.

Daniel Sturridge alifunga mara mbili wakati Liverpool ikiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Aston Villa katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Anfield na kutoa nafuu kwa kocha wa timu hiyo Brendan Rodgers.

No comments:

Post a Comment