Friday 18 September 2015

Mwanafunzi demu atoboa kuwa na uhusiano na mwalimu wakike



NEW YORK, Marekani
MAMLAKA ya New York yameanzisha uchunguzi kuhusu madai kuwa mwalimu mkuu msaidizi wakike alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi wakike.

Mkuu huyo msaidizi, Pelagia Papoutsis,mwenye umri wa miaka  33, aliondolewa mkukumku kutoka katika shule ya sekondari ya William Cullen Bryant kabla ya kuanza kwa vipindi mapema mwezi huu.

Papoutsis,mwalimu wazamani wa hisabati katika shule iliyopewa jina la utani la "Pelly," alipandishwa cheo hadi mwalimu mkuu mnsaidizi mwaka jana. Inaelezwa kuwa mwalimu huyo alikuwa karibu na mkuu wake Namita Dwarka, kwa mujibu wa  taarifa.

Mwanafunzi huyo wazamani anasema kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Papoutsis. Madai yaliyotolewa baada ya mwanafunzi huyo kuzungumza katika facebook na mwalimu wa gym Peter Maliarakis.

Maliarakis alichangia ujumbe huo na gazeti la New York Post.
Pelly aliuwa na mahusiano mabaya na mwanafunzi, aliandika mwanafunzi ambaye jina lake halikujulikana. Mimi nilikuwa shahhidi wa kwanza kwa sababu mimi nlihusika.

Mwanafunzi huyo pia katika ujumbe wake kwa Maliarakis akisema kuwa mkuu wa shule alikuwa akijua tatizo hilo lakini “hakulifanyia kzi” na hakufanya kitu chochote.

Maliarakis aliliambia gazeti la The Post: alisema uhusiano wao ulitokea wa mwaka wa mwisho. Alikuwa na umri wa miaka 17, na aliendelea hata baada ya kumaliza shule.

Tangu umri wa miaka 17, uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi mwenye umri huo halikuwa shitaka la jinai lakini mtu anaweza kuachishwa kazi ya ualimu mkuu msaidizi.

Regina Romain, msemaji wa Richard Condon, kamati maalum ya uchunguzi kwa shule za mjini, alithibitisha kuwa uchunguzi unaendelea. Alisema kuwa taarifa ya uchunguzi huo itachapishwa katika tarehe za usoni.

No comments:

Post a Comment