Saturday 19 September 2015

Wananchi wa Finland watoa viatu vya mamilioni kwa Riadha Tanzania


Kaimu Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Ombeni Zavalla (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Liike, Ari Koivu baada ya kukabidhiwa maboksi 15 ya zaidi ya jozi 400 za viatu vilitolewa na wananchi wa Finland kwenye Uwanja wa Taifa wiki hii.

 Na Mwandishi Wetu
RIADHA Tanzania (RT), wiki hii ilipokea jozi za viatu 450 zenye thamani ya sh. 45,000,000 kutoka kwa wananchi wa Finland.

Viatu hivyo vitasaidia katika maandalizi ya wanariadha wa Tanzania kushiriki mashindano mbalimbali yatakayofanyika nje ya nchi.
 
Akikabidhi viatu hivyo, Ari Koivu ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa wa taasisi ya Toiminnanjohtaja alisema kuwa, viatu hivyo pamoja na samani za ofisi vimetolewa na watu wa Finland ili kusaidia maendeleo ya michezo hapa nchini.

Alisema kuwa ameamua kutafuta vifaa hivyo kwa RT kutokana na mapenzi yake kwa Tanzania ili kuendeleza michezo na hasa riadha nchini.

Mbali na RT pia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kitivo cha Sayansi ya Michezo, baadhi ya shule za msingi na sekondari za Mtwara na Lindi nazo zimefaidikana msaada kutoka Finland, ambao ni tofauti na ule waliopewa RT.
 
Alisema kuwa mpango wa maendeleo ya michezo mikoa hiyo ya kusini utafaidika na msaada huo.
 
Kaimu Katibu Mkuu wa RT, Ombeni Zavalla alisema kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka kwani sasa wanajiandaa kuanza mazoezi kwa ajili ya mashindano mbalimbali ikiwemo Michezo ya Olimpiki itakayofanyika Rio, Brazil mwakani.

Alisema kuwa viatu hivyo vitawasaidia sana wanariadha kujiandaa vizuri kwa ajili ya mashindano mbalimbali, ambapo aliwataka wadau wengi kujitokeza kusaidia mchezo huo.


Ari Koivu (kulia) akimkabidhi jozi ya viatu mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Riadha Tanzania (RT), Rehema Killo `Mbeya wa Mtaa'.
Zacahria Gwandu, mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya RT akipokea jozi yake.



Add caption
Waandishi wa habari nao walipata mgao wa viatu na wengine jezi hivyo kutoka Finland.



Dk. Hamad Ndee (katikati) wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa mgao wa chuo hicho.

Add caption

No comments:

Post a Comment