Monday 24 April 2017

Wavu wa Muungano waanza kwa kasi Dar

Na Mwandishi Wetu
MASHINDANO ya Klabu Bingwa ya mpira wa wavu ya Muungano yalianza juzi kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mechi hizo za ufungunguzi, Mafunzo ya Zanzibar iliifunga Kinyerezi kwa seti 3-0 huku Chuo wakiitambia Kigamboni kwa seti 3-2.
Makongo waliipeleka puta Polisi Zanzibar kwa seti 3-1 huku Kinyerezi wakipoteza tena dhidi ya Chui pale walipofungwa 3-1.


Katika mchezo mwingine, Mafunzo waliifunga Victory kwa seti 3-0 na Jeshi Stars waliwafunga Polisi Zanzibar kwa seti 3-0.

No comments:

Post a Comment