Friday 14 April 2017

Mourinho aponda kiwango cha wachezaji wake baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Anderlecht

BRUSSELS, Ubelgiji
KOCHA wa Manchester United Jose Mourinho amekilaumu kikosi chake kwa washambuliaji `kuchemka’ baada ya Anderlecht kufanikiwa kuifunga bao la kusawazisha katika mchezo wa kwanza wa robo fainali Ligi ya Ulaya.

Man United ilikuwa mbele kwa bao 1-0 katika mchezo huo uliopigwa nchini Ubelgiji hadi pale katika dakika ya 86 wakati wenyeji waliposawazisha baada ya kulifikia lango hilo mara moja.
“Kama ningekuwa beki wa Manchester United ningeshangazwa sana na washambuliaji, “alisema Mourinho.

Henrikh Mkhitaryan alipata nafasi nzuri ya kuifungia Manchester United katika dakika ya 36, lakini hayo ndio yalikuwa mafanikio mazuri zaidi katika mashuti 16 yatimu hiyo waliyopiga kwa mpinzani wake.

Wageni wako pointi nne nyuma ya wapinzani wao Man City waliopo katika nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu ya England,ambapo wamefunga mabao 46.

Chelsea, Tottenham, Liverpool, Manchester City na  Arsenal wote kila mmoja tayari imefunga mabao zaidi ya 60.

Zlatan Ibrahimovic ndiye mchezaji anayeongoza kwa kufunga mabao katika timu hiyo baada ya kufunga mabao 28 katika mashindano yote, lakini Mkhitaryan na Juan Mata wanamfikia endapo ukilinganisha mabao yao yote.

"Ni matatizo hay ohayo, “aliongeza Mourinho. "Tulitawala mchezo, na tulipata nafasi, lakini tlishindwa kufunga mabao ya kutosha.


"Katika lugha yangu dhaifu ya Kiingereza neno zuri la kusema sio zaidi ya kuchemka. Tunatakiwa kuwa makini

No comments:

Post a Comment