Wednesday 19 April 2017

Waandaaji Ngorongoro Marathon watangaza zawadi nono za washindi wa mbio hizo za 10

Na Mwandishi Wetu
WAANDAAJI wa mbio za 10 za Ngorongoro Marathon wametangaza zawadi za washindi, imeelezwa.

Mbio hizo zimepangwa kufanyika Aprili 29 kuanzia katika lango kuu la kuingilia na kutokea katika Hihadhi ya Bonde la Ngorongoro mkoani Arusha.

Kwa mujibu wa mmoja wa waratibu wa mbio hizo za kimataifa Meta Petro, washidi kwa upande wa wanaume na wanawake  wapata zawadi sawa.

Petro alisema kuwa mshindi wa kwanza ataondoka na sh Milioni 1, wakati yule wa pili ataenda nyumbani na sh 500,000, huku watatu atapewa 250,000 na wanne sh 100,000.

Alisema maandalizi yanaendelea na yamefikia vizuri kwani jana alikuwa mjini Arusha akishughulikia medali za washindi na zawadi zingine.

Tayari Kampuni ya Vinywaji  baridi ya Bonite Bottlers na Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro wamekubali kudhamini mbio hizo.

Petro aliwataka watu, taasisi na makampuni kujitokeza kudhamini mbio hizo kwani nafasi bado ziko.

Pia aliwataka wanariadha kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo ambazo mwaka huu zinaendeshwa chini ya waandaaji wapya, ambapo kauli mbiu ni Kimbiza Jangili.

Mbio hizo zinalengo la kuwawezesha wananchi kuhusu kupiga vita mauaji ya tembo, faru, twiga, simba na wanyama wengine ili kulinda vivutio vya utalii.

No comments:

Post a Comment