Wednesday 19 April 2017

Klopp kumalizia kazi yake ya ukocha Liverpool

LONDON, England
JURGEN Klopp anasema kuwa haitakuwa ajabu ikiwa Liverpool ndiko patakuwa mahali pake pa mwisho kufanya kazi ya ukocha.

Klopp, ambaye klabu zake mbili alizowahikufundisha ni Mainz na Borussia Dortmund, alitua Anfield Oktoba mwaka 2015 ambako alisaini mkataba wa miaka sita katika kipindi kilichopita cha majira ya joto.

Na anasema kuwa anapendelea mkataba wa muda mrefu ambao utamuwezesha kutotaka kazi nyingine wakati muda wake utakapomalizika Merseyside.

Lakini anakiri wakati shinikizo la kushinda mataji likiongezeka, huku Liverpool ikiwa na ukame akirejea nyuma mwaka 2012 walipotwaa taji la Kombe la Ligi na hawajawahi kushinda lile la Ligi Kuu tangu mwaka 1992/93.

Klopp alisema: "Sitaweza kuwa katika kazi katika klabu 10 tofauti mara nitakapomaliza kazi yangu ya ukocha.

No comments:

Post a Comment