Friday 21 April 2017

Simbu kuonekana live DStv London Marathon

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Multchoice-Tanzania kupitia kisimbuzi cha DStv wataonesha mubashara mbio za Marathon za London, ambazo Mtanzania Alphonce Simbu atashiriki.

Macho na masikio ya watanzania yataelekezwa jijini London, kumshuhudia mwanariadha huyo akifanya vitu vyake katika mbio hizo kubwa.

Mbio hizi zitashirikisha wanariadha nyota duniani, ambao watawania kitita cha zaidi ya sh Milioni 200 zitakazotolewa kwa mshindi wa kwanza.

Wanariadha nyota watakaoshiriki mbio hizo ni wale kutoka Kenya, Ethiopia na Eritrea.
Mashindano hayo yataonekana Mubashara kupitia king’amuzi cha DStv  katika chaneli namba 209 ya SuperSport (SS9) kuanzia saa tano asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande alisema kuwa king’amuzi maarufu cha DStv kitaonesha mbio hizo ubashara `live’ nakuwawezesha watu kuona moja kwa moja.

“Wakati wote DStv imekuwa kinara katika kuwahakikishia watanzania wengi uhundo wa aina yake hususan katika ulingo wa michezo na burudani na kwa mara nyingine tena tunauwezesha umma wa watanzania kushuhudia tukio hilo muhimu, ambapo balozi wetu Simbu anatuwakilisha katika mashindano makubwa ya riadha,” akisema Maharage.

Simbu ambaye pia ni Balozi maalum wa DStv, ni Mtanzania wa kwanza kushinda medali ya dhahabu katika mashindano maarufu ya Standard Chartered Mumbai Marathon.

Katika mbio hizo za kesho, Simbu anatarajia kuwapa wakati mgumu wanariadha nyota duniani watakaoshiriki mbio hizo.

Multichoice Tanzania inamdhamini Simbu kwa muda wa mwaka mzima kwa lengo la kufanikisha maandalizi yake ya kushiriki mashindano ya Dunia yatakyofanyika jijini London Agosti.


Udhamini huo wa DStv ulianza tangu mwaka jana, ambapo mwanariadha huyo amekuwa akipatiwa posho ya kujikimu pamoja na kusaidia kambi yake ya mazoezi.

No comments:

Post a Comment