Friday 21 April 2017

Man United, Celta Vigo nusu fainali Ligi ndogo uefa

ZURICH, Uswisi
TIMU ya Manchester United itakutana na Celta Vigo ya Hispania katika mchezo wa nusu fainali wa Ligi ya Ulaya.

Klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya England imeshinda mara tatu taji hilo la Ligi ya Ulaya.

Timu ya Uholanzi ya Ajax, ambao ni washindi wa mwaka 1992, itakutana na timu ya Ufaransa ya Lyon katika mchezo mwingine wa nusu fainali.

Mechi za kwanza za nusu fainali zitachezwa Mei 4 huku zile za marudiano zitapigwa Mei 11, wakati fainali ya mashindano hayo itafanyika Mei 24 Stockholm, Sweden.

Kocha wa Man United Jose Mourinho alishinda taji hilo akiwa na Porto mwaka 2003 na atacheza na klabu ya La Liga ya Celta, ambayo haijawahi kushinda taji kubwa la Ulaya.

Ajax, ambayo iliifunga Schalke 4-3 kwa ushindi wa jumla ili kutinga nusu fainali, ina uzoefu katika mashindano ya Ulaya.

Timu hiyo imeshinda taji la Ubingwa wa Ulaya mara nne huku nyuma na Ligi ya Ulaya mara moja, ikiifunga Torino katika fainali ya mwaka 1992.

No comments:

Post a Comment