Wednesday 19 April 2017

Kocha Bayern Munich alina na mwamuzi Kassai

MADRID, Hispania
KOCHA wa Bayern Munich Carlo Ancelotti amesema mwamuzi Viktor Kassai hakuwajibika ipasavyo katika mchezo wa robo fainali wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na ametaka kuanza kutumika mara moja teknolojia ya video.

Kiungo wa Bayern Arturo Vidal alitolewa baada ya kuoneshwa kadi mbili, wakati nyota wa Real Madrid,  Cristiano Ronaldo akifunga katika muda wa nyongeza akiwa katika eneo la kuotea wakati mabingwa hao wa Ulaya wakisonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 6-3 jana.

Tulikuwa tukijia kila kitu wakati tukienda katika mchezo huu isipokuwa mwamuzi tu, “alisema Ancelotti.

"Huwezi kuamua timu inayokwenda nusu fainali kwa mtindo kama huu. Haiwezi kutokea katika kiwango hiki.”
Ancelotti, ambaye ni kocha wazamani wa Madrid, pia alisema kuwa kocha wa Real Zinedine Zidane alikubaliana na tathmini yake kuhusu mwamuzi huyo wa Hungary kushindwa kumudu mchezo huo kwenye Uwanja wa Bernabeu.

"Mwamuzi hakuwa kabisa katika mchezo na hakufanya kazi yake, “alisema Ancelotti.
"Sifikiri kama Real Madrid ilikuwa na ushawishi wowote kwa waamuzi. Waamuzi usiku huu wamechemsha, nilikuwa shishabikii matumizi ya teknolojia ya video, lakini sasa nakiri kuwa inahitajika.”

Teknolojia ya goli inaamua kama mpira umevuka mstari, ambapo ilianza kutumika katika Ligi kuu msimu wa mwaka 2013-14 na Bundesliga walianza kutumia kuanzia mwaka 2015-16.

Na Uingerea pia wanatarajia kutumia videoa kwa ajili ya kumsaidia mwamuzi kubadili maamuzi yake, ambapo hatua hiyo inatarajia kuanza katika kampeni za mwaka 2017-18.

Mwenyekiti wa Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge alimtuhumu Kassai kwa “kuharibu mchezo.”

Alisema: "Ni jambo linalojia hasira kwa mwamuzi kushindwa kutoa maamuzi ya haki….”
"Mchezo ulikuwa mzuri, lakini kwa bahati mbaya mwamuzi alitoa maamuzi ambayo ni wazi ndio yaliyotugharimu. Mwamuzi ndiye aliyeharibu mchezo.”

Katika mchezo huo, Cristiano Ronaldo alifunga mabao matatu `hat-trick’ wakati mabingwa watetezi Real Madrid wakiipiku kitata Bayern Munich katika muda wa nyongeza na kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

`Hat-trick’ ya Ronaldo imemfanya mchesaji huyo kuwa wa kwanza kufikisha mabao 100 katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.


Katika usiku huo, majirani wa Real Atletico nao walitinga nusu fainali ya mashindano hayo baada ya kutoka sare ya 1-1 na Leceister City na kushinda kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya kushinda 1-0 mchezo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment