Friday 28 September 2018

TAA Yaunga Mkono Tamasha la Urithi Wetu, Yatoa Fulana 100


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Richard Mayongela (kushoto) akimkabidhi moja kati ya fulana 100, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Prof. Audax Mabula (kulia), zilizotolewa na TAA kwa ajili ya Tamasha la Urithi Wetu kwa mkoa wa Dar es Salaam litakaloanza Oktoba Mosi, 2018, katika Kijiji cha Makumbusho ya Taifa, jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), katika kuunga mkono Tamasha la Urithi Wetu, imekabidhi fulana 100 katika hafla iliyofanyika Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Richard Mayongela alisema leo kuwa, wanaunga mkono tamasha hilo kwani linatangaza utalii wa nchini  na alikabidhi fulana hizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho ya Taifa, Professor Audax Mabula katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof. Audax Mabula (Kulia) leo akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa Tamasha la Urithi Wetu kwa mkoa wa Dar es Salaam, katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, jijini Dar es Salaam. kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela.

 Tamasha hilo ambalo lilizindulia mjini Dodoma mwezi huu, litafanyika jijini Dar es Salaam Oktoba Mosi katika Makumbusho ya Taifa, ambapo watu kibao wanatarajia kuhudhuria kabla ya kufanyika Zanzibar na baadae mikoa mingine.

Pia TAA imetangazwa kuwa mshirika wa tamasha hilo kwa ajili ya kutangaza utalii wan chi hiyo, ambapo mamlaka hiyo imeahidi kutangaza tamasha hilo katika viwanja vyake nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Richard Mayongela (katikati), Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof. Audax Mabula (kulia) na Mratibu wa Tamasha la Urithi Wetu Dk. Emannuel Bwasiri (kushoto) kwa pamoja wakionesha aina tatu za tisheti kati ya 100 zilizotolewa na TAA, kwa ajili ya Tamasha la Urithi Wetu kwa mkoa wa Dar es Salaam, katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, jijini Dar es Salaam.

Mayongela aliongeza kusema kuwa wameamua kujihusisha na tamasha hilo kwa kuwa viwanja vya ndege ni njia kubwa ya watalii kungia nchini, hivyo ni muhimu kujihusisha na tamasha hilo, ambalo lilizinduliwa na  Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Kama mchango wetu katika tamasha hili, TAA inawapa waandaaji wa Tamasha la Urithi nafasi ya kujitangaza katika viwanja vyetu vyote vya ndege ili kusaidia kuutagaza utalii na kufanikisha kuingia kwa watalii nchini, “alisema Mayongela.

Tamasha hilo ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka, linaandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, ambalo lilizinduliwa rasmi Septemba 15 mjini Dodoma na likiwa na lengo la kuongeza idadi ya watalii nchini kutoka milioni 1.3 mwaka jana ma kuongezeka zaidi.

Aidha, marais watatu wazamani wa Tanzania ni miongoni mwa watu walioalikwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kuhudhuria tamasha hilo la Oktoba Mosi.

Baada ya Dar es Salaam, Prtofesa Mabula alisema kuwa tamasha hilo litatua Jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheikh  Amri  Abeid  na Karatu, ambako ni njia kuu ya kuingilia katika Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro na Serengeti kuanzia Oktoba 8  hadi  13 

No comments:

Post a Comment