Wednesday 19 September 2018

Atletico Madrid Yatoka Nyuma na Kuifunga Monaco


MONACO, Ufaransa
TIMU ya Atletico Madrid ilitoka nyuma na kuifunga Monaco 2-1 katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya uliofanyika hapa.

Wenyeji Monaco ndio walikuwa wa kwanza kupata bao la kongoza kupitia kwa Samuel Grandsir baada ya kutumia vizuri makosa ya uzuiaji yaliyofanywa na wote, Saul na Angel Correa.

Diego Costa aliisawazishia Atletico Madrid baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Antoine Griezmann na kufunga bao huku Jose Gimenez akifunga kwa kichwa kocha ya Koke na kuwapatia wageni uongozi wa mchezo huo.

Lakini Atletico, huku kocha wake Diego Simeone akiwa jukwaani, nusura wafungwe bao katika dakika za majeruhi wakati mpira wa kichwa uliopigwa na Kamil Glik ulipopaa juu ya lango.

Kocha huyo Muargentina alikuwa akitumikia mechi yake ya mwisho baada ya kufungiwa mechi nne za Ulaya, baada ya kufanya kosa katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Ulaya walipocheza dhidi ya Arsenal.

Winga Thomas Lemar, aliyesajiliwa kwa pauni Milioni 62 akitokea Monaco, alipata mapokezi mazuri wakati alipoingia katika kipindi cha pili akiichezea Atletico.
Wachezaji wa Monaco.
Katika mchezo mwingine wa Kundi A, Borussia Dortmund iliondoka na pointi zote tatu katika kundi lake baada ya kuifunga Club Brugge 1-0 shukrani kwa bao la ushindi la dakika za mwisho la Christian Pulisic katika dakika ya  20. Chipukizi wa  Dortmund, Jadon Sancho alikuwa akicheza kwa mara ya kwanza mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Katika Kundi C, mashabiki 50,.000 walishuhudia timu ya Red Star Belgrade ikitoka suluhu na kikosi cha kocha wa Napoli, Carlo Ancelotti katika mchezo wao wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya tangu mwaka 1992.

Katika mchezo mwingine, kipa wa FC Porto Iker Casillas amekuwa mchezaji wa kwanza katika kampeni tofauti 20 za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya timu yake kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Schalke katika mchezo wa Kundi D, huku Galatasaray ikiifunga Lokomotiv Moscow 3-0.

No comments:

Post a Comment