Sunday 9 September 2018

Mkurugenzi Mkuu TAA, Bw. Mayongela Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Mfanyakazi JNIA




Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Richard Mayongela akimpa pole mjane wa Marehemu Bw. Charles Salim nyumbani kwake Chang’ombe jijini  Dar es Salaam.
Na MwandishiWetu
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela leo meongoza mamia ya Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kuuaga mwili wa Ofisa Usalama Mwandamizi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), aliyefarikijuzi Tarehe 6/9/2018 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kupatwa na shambulio la moyo.

Akisoma wasifu wa marehemu, Bw. Mayongela amesema Mamlaka itaendelea kushirikiana na familia ya marehemu, ambaye ameacha mjane na watoto wawili.
“TAA kama mwajiri wa marehemu tumefanikisha shughuli zote za hapa msibani natupo tayari kushirikiana na familia ya marehemi hata baada ya msiba huu kumalizika, "alisema Mayongela.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Bw. Richard Mayongela akitoa salamu za rambimbi katika msiba wa Bw Charles Salim Chang'ombe Jijini Dar es Salaam.
Bw.Mayongela amesema marehemu wakati wa uhai wake alifanyakazi kwa ufanisi mkubwa, hivyo ameacha pengo kubwa kwa taasisi.

Naye msemaji wa Familia, Bw. Herbert Semwaiko aliishukuru TAA kwa ushirikiano walionesha tangu kuugua ghafla kwa marehemu hadi kufariki kwake.

“Sina maneno zaidi ya kusema pamoja na Kiswahili ni lugha pana zaidi, ila nasema asante sana tunawashukuru kwa ushirikianowenu mliouonesha, ambapo mmetusaidia kuanzia mwanzo wa ugonjwa wa ghafla hadi kufariki kwake kijana wetu, Charles, "anasema Bw. Semwaiko.

Kwa upande wake, Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Anglikana, Daniel Mhando katika ibada yake fupi ya kumuombea marehemu aliwataka waombolezaji kumuombea katikasafari ya mwisho atazikkwa Jumapili Septemba 9, 2018 wilayani Muheza mkoani Tanga.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wakiwa na Mkurugenzi Mkuu (watatu kulia), Bwa. Richard Mayongela wakiwa pembeni ya jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Ofisa Usalama Mwandamizi, Bw Charles Salim tayari kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho.
Marehemu alizaliwa tarehe Oktoba 3, 1963 na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya Kibasila Jijini Dar es Salaam na baadae elimu ya sekondari katika shule ya Hengongo mkoani Tanga, ambapo alihitimu kidato cha nne mwaka 1983 na mwaka 1984 aliajiriwa serikalini na kupangiwa kazi Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Dar es Salaam, kama Ofisa Usalama, na mwaka 2015 alipandishwa cheo na kuwa Ofisa Usalama Mwandamizi.
Watoto wa aliyekuwa Ofisa Usalama Mwandamizi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Charles Salim, James Charles (Mwenye fulana nyeusi) na Lissa Charles (aliyefunga kitambaa kichwani) mara baada ya ibada fupi wakiwa na Mkurugenzi Mkuuwa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wa pili kulia) nyumbani kwao Chang’ombe jijini  Dar es Salaam.
 Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe. Amina.

No comments:

Post a Comment