Wednesday 19 September 2018

Messi Apiga Hat-trick Barcelona Ikiifunga PSV 4-0


BACELONA, Hispania
LIONEL Messi alifunga hat-trick yake ya 48 katika historia ya soka wakati Barcelona ikiwasambaratisha mabingwa wa Uholanzi, PSV Eindhoven kwa mabao 4-0 katika mchezo wa ufunguzi wa hatua ya makundi wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Nahodha huyo wa Barca alianza mbio zake hizo za kufunga mabao matatu katika mchezo huo pale alipofunga bao la kwanza kwa mpira wa adhabu kabla shuti la Luis Suarez la umbali wa kama meta 20 kugonga mtambaa panya.

Ousmane Dembele, ambaye yuko katika kiwango kizuri cha uchezaji aliwatoka mabeki wawali na kuiwezesha Barcelona kupata bao lake la pili akipiga mpira mkutoka nje ya boksi.
Messi alifunga bao la tatu baada ya kupata pasi pasi ya juu kutoka kwa Ivan Rakitic kabla beki wa Barcelona, Samuel Umtiti kutolewa nje baada ya kupewa kadi ya pili ya njano.

Licha ya kuwa 10 uwanjani, Barcelona walipata bao la nne wakati Suarez hajampatia Messi mpira, ambaye aliupiga na kumpita kipa Jeroen Zoet kutoka umbali wa kama meta 15.

Katika mchezo m,wingine wa Kundi B ulishuhudia Inter Milan ikitoka nyuma na kuichapa Tottenham 2-1 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa San Siro.

Messi, ambaye sasa ni nahodha wa Barcelona baada ya kuondoka kwa Andres Iniesta, anaonekana kuwa kuweka kando kufanya vibaya katika Kombe la Dunia nchini Urusi, baada ya kufunga mara moja tu katika fainali hizo katika hatua ya 16 bora.

Sasa mchezaji huyo amefunga mabao saba katika mechi sita msimu huu, na alikaribia kufunga pale alipopiga mpira wa adhabu katika kipindi cha pili na kutengeneza nfasi nzuri kwa Suarez na Roberto.

Mabao yake yote matatu yalikuwa mazuri. La kwanza alifunga kwa mkwaju wa adhabu likiwa ni la nane kufunga kwa staili hiyo, baada ya kupiga mpira uliojaa katika kona ya juu ya upande wa kulia wa lango.

Hadi sasa amefunga mabao 104, zikiwemo hat-trick nane katika mashindano na amepachika mabao katika mechi mfululizo 14 za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, akifikia rekodi ya gwiji wa Real Madrid, Raul.

MWAKA WA BACELONA?
Barcelona kwa miaka mitatu mfululizo imekuwa ikitolewa katika hatua ya robo fainali, huku maadui zao Real Madrid wakitwaa taji hilo katika vipindi hivyo vyote.

Wachezaji wa Barca katika kipindi hiki cha majira ya joto walizungumzia kuhusu umuhimu wa Ligi ya Mabingwa kwao wakati wakijaribu kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2015.

Msimu uliopita washindi hao wa mataji mawili wa Hispania walionekana wako shapu dhidi ya wapinzani wao baada ya kushinda mechi saba huko nyuma na alifunga mabao 13 katika mechi mbili huko nyuma, ingawa PSV walikuwa wazuri zaidi tofauti na matokeo yalivyokuwa.

Wakianza na wachezaji tisa kati ya 11 waliocheza na Roma msimu uliopita, Barceloma ilianza mchezo huo kwa nguvu huku Philippe Coutinho, akiichezea timu hiyo kwa mara ya kwanza katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, alipiga kichwa mpira wa krosi iliyochingwa na Suarez.

Zoet alifanya kazi kubwa kuokoa michomo ya wazi kutoka kwa Sergi Roberto na Coutinho.

HISTORIA YA MESSI
Barcelona imeshinda mechi 25 kati ya 27 zilizopita za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya walizocheza kwenye uwanja wao wa Nou Camp, wakitoka sare mbili. Na kwa mara ya mwisho walipoteza mchezo kwenye uwanja huo, Mei 2013 walipocheza dhidi ya Bayern Munich (3-0).

PSV Eindhoven haijashinda mechi zake tisa zilizopita za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya (wakitoka sare mara nne na kupoteza tano).

Messi amefunga katika mechi tofauti 30 za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya, huku akipitwa na Raul (33) na Cristiano Ronaldo (32) wakifunga dhidi ya wapinzani tofauti tofauti.
Amefunga mara nane kwa mikwaju ya adhabu mwaka huu.

Muangetina huyo amefunga hat-trick nyingi zaidi kuliko mchezaji yeyote katika historia ya Kombe la Ulaya (8). Ameifungia Barcelona hat-trick 42 na sita ameifungia timu yake ya taifa ya Argentina.

NINI KIFUATACHO?
Barcelona itakuwa mgeni katika mchezo wa marudiano utakaofanyika kwenye Uwanja wa Wembley wakati itakapokabiliana na Tottenham katika mchezo wa raundi ijayo, huku PSV itakuwa mwenyeji wa Inter Milan – zote zitafanyika Jumatano, Oktoba 3.

No comments:

Post a Comment