Tuesday 16 June 2015

Siku ya Mtoto wa Afrika ilivyofana Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam

Wanafunzi wa shule ya msingi ya Madenge wakiendesha Bunge maalum la watoto wakati wakiadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika leo kwenye viwanja vya Mwembe Yanga.
Baadhi ya washiriki wa Siku ya Mtoto wa Afrika mkoa wa Dar es Salaam kwenye viwanja vya Mwembe Yanga leo Jumanne, Juni 16.

Spika wa Bunge la Watoto, Zubeda Yussuf  (wa pili kulia), wa shule ya msingi Madenge iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam leo., akitoka baada ya kuendesha kikao wakati wa Siku ya Watoto Mwembe Yanga.
Wanafunzi wakicheza mchezo wa kuigiza kuhusu ndoa za utotoni wakati wa kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika leo katika viwanja vya Mwembe Yanga.
Wanafunzi wakicheza wakati wa Siku ya Mtoto wa Afrika jijini Dar es Salaam jana.

No comments:

Post a Comment