Wednesday 24 June 2015

Covenant Bank yaipatia Chaneta sh. Milioni 40 kwa safari ya Botswana

*Ni tiketi 20, mabegi na suti za michezo kwa ajili ya mashindano ya Afrika


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Covenant. Sabetha Mwambenja (kushoto) akizungumza kabla ya kukabidhi tiketi za ndege kwa timu ya Taifa Queens. Kulia ni nahodha wa timu hiyo Sophia Komba.

Mwenyekiti wa Chaneta Annie Kibira (kushoto) akizungumza wakati wa kukabidhiwa tiketi za ndege na Covenant Bank leo asubuhi.
Ofisa Michezo wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Allen Alex  akizungumza wakati wa hafla hiyo.

Nahodha wa timu ya taifa ya netiboli, Taifa Queens, Sophia Komba.
 



Mkurugenzi wa Coenant Bank (kushoto) akimkabidhi tiketi mmoja wa wachezaji wa Taifa Queens.

Na Cosmas Mlekani
BENKI ya Covenant leo imetoa tiketi 20 za ndege, mabegi na suti za michezo kwa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) ili kuiwezesha timu ya Taifa Queens kwenda Gaborone Botswana kushiriki mashindano ya Afrika.

Mashindano hayo yanaanza Jumamosi na Taifa Queens inaondoka Ijumaa na wachezaji 17 na viongozi watatu tayari kwa mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Benki hiyo ya wanawake ya Tanzania imetoa jumla y ash. Milioni 40 kwa ajili ya tiketi na vifaa hiyo vingine ambavyo itatumika na timu hiyo ikiwa nchini Botswana.

Akizungumza wakati wa kukabidhi tiketi hizo katika Makao Makuu ya benki hiyo Kijitonyama jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Sabetha M.J Mwambenja alisema kuwa wameisaidia Taifa Queens ili kuwawezesha kushiriki mashindano hayo.

Alisema timu hiyo inaundwa na wanawake hivyo ni moja ya jukumu lao kuwawezesha wanawake kufikia malengo yao kwa njia tofauti.

Mwakilishi wa Wizara ya Kazi, Vijana Utamaduni na Michezo Allen B. Alex liishukuru benki hiyo kwa kubeba `msalaba wa wizara hiyo ambayo ni jukumu lake kuvisaidia vyama vya michezo.

Naishukuru benki ya Covenant kwa kuchukua msalaba wa serikali wa kuvisaidia vyama vya michezo kuisaidia Chaneta kupeleka timu Namibia alisema Alex.

Alizitaka tasisi zingine kuiga mfano wa Cevenant Bank wa kusaidia jamii.

Mwenyekiti wa Chaneta Annie Kibira aliishukuru benki hiyo hasa mkurugenzi wake (Mwambenja) kwa kukubali kuisaidia Chaneta licha ya kuombwa kwa muda mfupi.

Nawapongeza Covenant na hasa dada yangu (Sabetha) kwa kukubali kutusaidia licha ya kuwasilisha maombi siku chache zilizopita alisema.

Naye nahodha wa timu hiyo Sophia Komba alisema kuwa, wamejiandaa izuri kwa ajili ya mchezo huo na wanatarajia kufanya vizuri katika mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment