Sunday 31 May 2015

Ufungaji wa tamasha la michezo la shule za Filbert Bayi ulivyosisimua Mkuza Kibaha

Soka lilipamba moto

Soka ilikuwa kivutio pia katika tamasha hilo la michezo ambalo hufanyika kila baada ya mwaka mmoja.

Ushindi mtamu!: Ofisa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Mwinga Mwanjala (kulia) akifurahia na mwalimu bao lililofungwa na timu ya shule ya msingi ya Filbert Bayi ya Kimara dhidi ya wenzao wa Kibaha. Timu hizo zilifungana 1-1.

Wanafunzi wa shule za msingi za Filbert Bayi nao walichuana hata katika soka pia.

Wazazi wenye watoto katika shule za Filbert Bayi wakitoana jasho katika kuvuta kamba.

Mchezo wa kuvuta kamba, haikuwa rahisi kushinda

Mkurugenzi wa shule za Filbert Bayi, Anna Bayi (kulia), akiteta jambo na msaidizi wake Eliberth wakati wa bonanza la michezo la shule hizo lililofanyika Mkuza, Kibaha.



Kumekucha mchezo wa kukimbiza kuku; kila mmoja akifikiria kitoweo endapo atamkamata jogoo hilo.



Mchezo wa kukimbiza kuku

Mchezo wa kukimbiza kuku uliwatoa jasho washiriki.

Mchezo wa kukimbiza kuku nao ulikuwepo katika tamasha hilo la michezo la shule zaFilbert Bayi.

Timu ya shule ya sekondari ya Filbert Bayi katika picha ya pamoja kabla hawajacheza na wenzao wa East Coast.

Timu ya soka ya shule ya sekondari ya East Coast katika picha ya pamoja.

Mgeni rasmi akikagua timu ya shule ya sekondari ya East Coast ya Pwani kabla haijacheza na Filbert Bayi Mkuza Kibaha.

Mgeni rasmi akiteta jambo na wachezaji wa timu ya shule ya sekondari ya East Coast na wale wa Filbert Bayi kabla ya kuanza kwa pambano la soka. Filbert Bayi walishinda 2-0.

Hata mchezo wa mbio za pikipiki ulikuwepo, mmoja wa waratibu Peter Mwita akiwaelekeza jambo baadhi ya washiriki hao.

Baadhi ya wakuu wa shule za Filbert Bayi wakati wa bonanza la michezo wakiteta jambo.

Uwanja mpya wa ndani wa shule za Filbert Bayi umekamilika na tayari umeanza kutumika wakati ukisubiri kufunguliwa rasmi wakati wowote.


No comments:

Post a Comment