Wednesday 13 May 2015

Barcelona yafungwa na Bayern, yatinga fainali Ulaya



 
BAYERN Munich, Ujerumani
MABINGWA wa Ujerumani, timu ya Bayern Munich jana usiku ilitupw nje ya mashindano ya ya Ligi ya Mabingwa Ulaya licha ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika mchezo wa pili wa nusu fainali.

Katika mchezo wa awali, Barcelona ilishinda 3-0 na hivyo timu hiyo ya Hispania imesonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 5-3.

Barca sasa itamsubiri mshindi wa jumla kati ya Juventus na Real Madrid kwa ajili ya kucheza fainali itakayofanyika baadae mwezi huu.

Katika mchezo wa kwanza, Juventus iliibuka na ushindi wa bao 2-1 ns timu hizo zinakutana leo Jumatano katika mchezo wa marudiano huko Madrid.

ikutane katika fainali. Juve ilishinda 2-1 katika mchezo wa kwanza.

Mabao ya Bayern katika mchezo huo wa jana usiku yalifungwa na Medhi Benatia dakika ya saba, Robert Lewandowski dakika ya 59 na Thomas Muller dakika ya 74, wakati ya Barca mabao yake yote yalifungwa na Neymar dakika ya 15 na 29.

No comments:

Post a Comment