Monday 11 May 2015

Duniani Kuna Mambo; Paka azaa mbwa nchini China



XUZHOU, China
MZEE mmoja wa Kichina alipigwa na butwaa baada ya kumsaidia paka wake kuzaa na mkubaini kuwa miongoni mwa vitoto vile kimoja wapo kilikuwa ni mbwa.

Mstaafu huyo anayejulikana kwa jina la Jia Weinuan akiwa amejipumzisha nyumbani kwake, alishuhudia paka wake mwenye umri wa miaka mitatu Niu Niu akizaa watoto watano.

Wakati akifanya ukaguzi wa karibu zaidi na kutoa huduma kwa mama paka huyo mzazi, Jia, mwenye umri wa miaka 74, alisema hakuamini macho yake wakati alipobaini miongoni mwa vitoto vile vilivyozaliwa na paka yule ni mbwa.

Alisema: "Nilifikiri kuna vitoto vitano vya mbwa wenye maumbo madogo, lakini badae nilipoangalia kwa ukaribu zaidi nilibaini viko vitano.

"Kwa maisha yangu yote, kamwe sijawahi kuona au kusikia mbwa na paka wakafanya mapenzi.

Jia, ambaye hana mbwa nyumbani kwake, alisema yeye na mkewe hawana maelezo zaidi kuhusu maajabu hayo.

Alisema haamini kama paka wake Niu Niu alikutana na mbwa-kwa sababu sio rahisi kuwapandisha wanyama hao.

Wiki moja kabla ya kuzaa, Niu Niu walimpeleka kwa rafiki yao kwa jili ya uangalizi wa karibu.

Lakini alisema kuwa rafiki yake huyo alimuweka paka huyo na wengine wakiume wawili, na imeendelea kuwaacha bila majibu yoyote.

Jia, kutoka jijini la Xuzhou, kaskazini ya China, alisema: "Hili tuki linachanganya sana.

"Nategemea vyombo vya habari vitaripoti tukio hili na bila shaka tutapata maelezo kamili kutoka kwa wanasayansi."

No comments:

Post a Comment