Tuesday 30 August 2016

DSTV ilivyoandaa chakula cha usiku na kuwapa zawadi wachezaji wa Tanzania walioshiriki Olimpiki ya Rio 2016

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akipokea bendera ya taifa kutoka kwa nahodha wa timu ya Tanzania iliyoshiriki Michezo ya 31 ya Olimpiki iliyofanyika Rio, Brazil, Alphonce Felix Simbu katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi akizungumza na Meneja Masoko wa MultiChoice- Tanzania, Furaha Samalu kabla ya kuanza kwa hafla ya kuwapongeza wachezaji walioshiriki Michezo ya Olimpiki ya rio 2016 katika hoteli ya Serena.
Baadhi ya wadau wa michezo waliohudhuria tafrija hiyo.


Rais wa TOC, Gulam Rashid akizungumza katika hafla hiyo.
Aliyekuwa Mkuu wa Msafara wa timu ya Tanzania iliyoshiriki Michezo ya Olimpiki ya Rio 2016, Suleiman Jabir.

Waziri sa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akimkabidhi tuzo mwanariadha Alphonce Felix Simbu baada ya kumaliza wa tano katika Michezo ya Olimpiki iliyomalizika hivi karibuni Rio, Brazil.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akimkabidhi zawadi mwanariadha Fabian Joseph aliyeshiriki Michezo ya 31 ya Olimpiki.

Kocha wa timu ya Tanzania ya riadha iliyoshiriki Michezo ya Olimpiki, Francis John akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
Meneja Masoko wa Multchoice-Tanzania, Furaha Samalu akipokea cheti cha shukrani kwa kazi nzuri iliyofanywa na kampuni yake kutoka kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye kilichotolewa na TOC. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania Maharage Chande.

Muogeleaji Hilal Hemed Hilal akipewa zawadi na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye.Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania, Maharage Chande.
 
 
Wachezaji walioshiriki Olimpiki 2016, viongozi wa michezo na wadau wengine wote walipata mlo wa usiku ulioandaliwa na Multchoice-Tanzania katika hoteli ya Serena.
 


No comments:

Post a Comment