Tuesday 24 May 2016

Upungufu wa sukari wasababisha kusimama kwa uzalishaji wa Coca Cola na kusababisha misururu ya kununua sukari Venezuela



Wananchi wa Vunezuela wakiwa katika mstari mrefu kwa ajili ya kunua bidhaa mbalimbali ikiwemo sukari iliyoadimika.

CARACAS, Venezuela
UPUNGUFU wa sukari umelazimisha Coca-Cola kusimamisha uzalishaji wa vinywaji nchini hapa kutokana na matatizo ya chakula na nishati.

Coke katika taarifa yake ilisema kuwa Venezuela kwa muda itasimamisha uzalishaji kutokana na upungufu wa mali ghafi.

Tangazo hilo limekuja baada ya kampuni hiyo kubwa ya vinywaji, Empresas Polar, kufunga kiwanda kutokana na upungufu huo mkubwa wa sukari.

Uchumi wa Venezuela umeporomoka kwa haraka kutokana na bei ya mafuta kuyumba.

Msemaji wa Coca-Cola alisema kuwa kampuni hiyo itaendelea kuzalisha vinywaji visivyo na sukari kama Coca-Cola Light (Diet Coke).
Uzalishaji wa miwa umeporomoka kutokana na kudhibitiwa kwa bei na kupanda kwa gharama za uzalishaji, pamoja na upatikanaji wa mbolea.

Matokeo yake, wakulima wengi wadogo wamehamia katika uzalishaji wa mazao mengine ambayo bei yake haidhibitiwi, ambayo pia huwapatia kipato kikubwa.

Venezuela ilitarajiwa kuzaliwa tani 430,000 za miwa mwaka 2016/17, badala ya tano 450,000 kwa miezi 12 iliyopita, na kuingiza tani 850,000 ya malighafi na sukari iliyokuwa tayari imeshatengenezwa kwa mujibu wa takwimu za USDA.

Matatizo ya kiuchumi yamesababisha wananchi wengi kujipanga katika misururu mirefu kwa saa kadhaa wakinunua mahitaji ya nyumbani.

No comments:

Post a Comment