Saturday 7 May 2016

Bayern Munich yatwaa taji la nne mfululizo Ujerumani baada ya kuifunga Ingolstadt 2-1



MUNICH, Ujerumani
BAYERN Munich leo wametwaa ubingwa wa Bundesliga kwa mara ya 26 huku ukiwa umebaki mchezo mmoja kabla ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya nchi hiyo huku mabao mawili ya Robert Lewandowski yaliiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ingolstadt.

Kikosi hicho cha kocha Pep Guardiola kimejifariji kwa ushindi huo baada ya juzi kutolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya katika nusu fainali kwa kutwaa kwa mara ya nne mfululizo taji hilo la Ujerumani la Bundesliga.

Lewandowski aliiweka mbele Bayern kwa bao la penalty kabla hajaongeza bao jingine kwatimu hiy kufuatia pasi ya Xabi Alonso.

Penalti ya Moritz Hartmanni ilifanya matokeo hayo kuwa 2-1 lakini imefanikiwa kutetea taji lake hiyo.

Kutawala Nyumbani
Borussia Dortmund ndio timu pekee inayoweza kukishika kikosi cha kocha Guardiola lakini kufungwa kwake bao 1-0 na Eintracht Frankfurt kuna maana kuwa Bayern Munich iko mbele kwa point inane mbele ya mpinzani wake mkubwa wakati akicheza mechi za wikiendi hii.

Guardiola ataanza kibarua chake kipya Manchester City katika kipindi hiki cha majira ya joto huku akiwa ametwaa mara tatu taji la Bundesliga katika misimu yake mitatu ya kuifundisha timu hiyo.
Kocha huyo wazamani wa Barcelona hakuwa katika furaha wakati mchezo hu ukianza kutokana na timu yake kutolewa na Atletico Madrid kwa sheria ya bao la ugenini katika michuano ya Ligi ya Mabingwa.

Lakini kocha huyo mwenye umri wa miaka 45 naye alikuwa na furaha kubwa wakati akishangilia na wachezaji wake baada ya filimbi ya mwisho dhidi ya Ingolstadt iliyopo katikati ya msimamo wa ligi baada ya kushinda mara 81 katika michezo 101 chini ya Guardiola.

No comments:

Post a Comment