Thursday 6 June 2019

Mbwana Samatta Anunuliwa kwa Bilioni 35 England

Mbwana Samatta (wa pili kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Genk ya Ubelgiji katika moja ya mechi za Ligi  Kuu ya nchi hiyo.

LONDON, England
BRIGHTON inaongoza mbio za klabu za Ligi Kuu kutaka kunsajili mshambuliaji wa mabingwa wa soka wa Ubelgiji Genk na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Samatta.

Timu iliyopanda daraja ya Aston Villa, Leicester, Watford pamoja na  Burnley, zote zinataka kumsajili mchezaji huyo kwa kiasi cha pauni milioni 12 (sawa na sh bilioni 35).

Na Samatta, mwenye umri wa miaka 26, anajua kuwa anataka kwenda kucheza soka katika Ligi Kuu ya England baada ya kufanya vizuri katika Ligi Kuu ya Ubelgiji msimu huu.

Mchezaji huyo alifunga mabao 23 na kuisaidia klabu yake ya Genk kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Ubelgiji pamoja na kutwaa tizo ya kiatu cha Ebeny, ambayo hutolewa kwa mchezaji bora wa Ubegiji kutoka Afrika.

Tuzo hiyo huko nyuma imewahi kuchukuliwa na Romelu Lukaku, Vincent Kompany na Michy Batshuayi.

Samatta ataiongoza Taifa Stars katika mashindano ya Mataifa ya Afrika, Afcon 2019, yatakayofanyika Misri mwezi huu, ikiwa ni mara ta kwanza kwa Tanzania kushiriki tangu ilipocheza kwa mara ya mwisho mwaka 1980.

Lakini baada ya kumalizika kwa mashindano hayo, Samatta anatarajia kuondoka Genk, ambayo alijiunga nayo Januari mwaka 2016 akitokea klabu ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ya TP Mazembe, na kwenda Ligi Kuu ya England.

Brighton imekuwa ikimfuatilia Samatta kwa muda na kocha wazamani Chris Hughton ambaye ni shabiki mkubwa, wakati Graham Potter naye pia amekuwa akimkubali mshambuliaji huyo.

Kocha mpya wa Brighton Graham Potter anataka kuimarisha kikosi chake kipya kwa ajili ya Ligi Kuu.

Samatta endapo atajiunga na Brighton atakuwemo katika ziara ya timu hiyo kabla ya kuanza kwa ligi ambayo itafanyika Austria kuanzia Julai 7 na itacheza mechi kadhaa za kirafiki.

No comments:

Post a Comment