Tuesday 4 June 2019

Arsenal, United Zawania Kumsajili Mchezaji wa PSG


LONDON, England
ARSENAL na Manchester United zinawania kumsajili mchezaji wa Paris Saint-Germain (PSG), Thomas Meunier (pichani) msimu huu, vyanzo vimeiambia ESPN FC.

PSG imeweka wazi mauzo ya mchezaji huyo ambayo itahitaji karibu pauni milioni 30 kwa mchezaji aliyebakiza miezi 12 kwenye mkataba wake.

Vyanzo vilisema, miamba hiyo ya Ligi Kuu tayari imeonyesha nia yao kwa mchezaji huyo.

Kocha wa Arsenal Unai Emery,  aliyemsajili Meunier PSG, yuko nyuma ya the Gunners kumuwania nyota huyo.

Vyanzo viliongeza, United na Arsenal zinajiandaa kupambana kwenye ligi ya Europa msimu ujao badala ya Ligi ya Mabingwa.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliliambia Le Parisien kuna klabu kubwa tano zimeonyesha muhitaji tangu Januari.

"PSG haijanambia kama inataka kuniuza,” alisema  Meunier. "Wanajua kwamba wananihitaji.”

"Kama klabu itaniambia 'sikiliza tunataka kukuuza, tunahitaji fedha’ basi sitacheza hapa msimu ujao.”

No comments:

Post a Comment