Tuesday 4 June 2019

Wateja Tigo Kujishindia Tiketi Kuishangilia Stars Misri

Mkuu wa Bidhaa na Huduma wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo, David Umoh (kulia) na Meneja wa Huduma za Ziada wa kampuni hiyo, Ikunda Ngowi wakati wa uzinduzi wa Promosheni ya SOKA LA AFRIKA  kwa ajili ya kujishindia tiketi za kwenda Misri kuishangilia Taifa Stars katika mashindano ya Mataifa ya Afrika, Afcon 2019. Hafla hiyo imefanyika Jijini Dar es Salaam leo.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu za Mkononi ya Tigo itapeleka mashabiki 10 wa soka kuishangilia timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon 2019, nchini Misri, imeelezwa.

Taifa Stars, itashiriki kwa mara ya kwanza fainali hizo baada ya kushiriki mara ya mwisho miaka 39 iliyopita, wakati mashindano hayo yalipofanyikia Lagos, Nigeria mwaka 1980 na tangu wakati huo imekuwa ikiishia katika hatua ya kufuzu.

Tigo wameanzisha promosheni ya Soka la Afrika ili kupata kupata watu 10, ambao mbali na kujishindia nafasi hizo za kwenda kuishangilia Taifa Stars ikicheza Afcon 2019, pia watapata nafasi ya kuwa mamilionea.
Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa Soka la Afrika jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Bidhaa na Huduma wa kampuni hiyo, David Umoh alisema kuwa wateja wa Tigo wanayo nafasi ya kujishindia safari ya kwenda Misri kushuhudia Kombe la Mataifa ya Afrika pamoja na zawadi za fedha taslimu.

Kampuni hiyo imetenga zaidi ya Sh Milioni 50 katika promosheni hiyo ya Soka Letu, ambapo pia kutakuwa na washindi 10, ambao watagharimiwa kila kitu kwenda kuishuhudia Taifa Stars katika michuano hiyo ya Afcon 2019.

“Tunaamini kwa kutumia mashindano haya, tunaweza kupata fursa nzuri kutoa habari, elimu na burudani kwa kutumia jukwaa la mawasiliano na huduma za kampuni hiyo katika kutumia huduma na bidhaa zetu, “alisema Umoh.
Meneja wa Huduma za Ziada wa Tigo, Ikunda Ngowi akizungum\za na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Promosheni ya SOKA LA AFRIKA uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkuu wa wa Bidhaa na Huduma wa kampuni hiyo, David Umoh.
Fainali za Afcon ni mashindano makubwa kabisa barani Afrika kwa timu za taifa, ambazo zinawaleta pamoja wachezaji wa Kiafrika wanaoshiriki ligi kubwa na zenye ushindani ndani na nje ya Afrika.

“Tunaamini itakuwa jambo zuri kwa wateja wetu kupata nafasi ya kwenda kushuhudia mashindano haya makubwa ikiwa ni pamoja na kushangilia timu yetu ya Taifa Stars itakayotuwakilisha. Tunawatakia kila la kheri, “aliongeza Umoh.

Alisema zaidi ya wateja 100 watashinda zawasi za fedha taslimu kila siku, wiki na kila mwezi kwa muda wa miezi mitatu katika shindano hilo, ambalo mshiriki atatakiwa kutuma neno SOKA kwenda 15670 ili kuweza kujibu maswali yanayohusu Afcon 2019.

Mashindano ya 32 ya Afcon 2019 yataanza Misri kuanzia Juni 21 hadi Julai 19 na Tanzania imepangwa Kundi C pamoja na Kenya, Senegal na Algeria na itaanza kampeni zake kwa kucheza dhidi ya Senegal.


No comments:

Post a Comment