Sunday 6 November 2016

MAISHA MAGIC BONGO YAZINDULIWA RASMI NA KUIPAISHA JUU BONGO MOVIES



Mgeni rasmi pamoja na waheshimiwa wengine wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguaji wa uzinduzi.
Na Mwandishi Wetu
MAISHA Magic Bongo kwa kushirikiana na maprodyusa wa filamu nchini wameleta mapinduzi  makubwa kwenye sanaa ya filamu za Kibongo.

Palikuwa na full shangwe na vifijo  kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam siku ya  Ijumaa, Novemba 4,  2016. Shangwe hii ni baada ya Maisha Magic Bongo kwa kushirikiana na Multichoice Tanzania kuzindua rasmi chaneli yao ya (160) Maisha Magic Bongo. Miongoni mwa waalikwa walikuwa waigizaji maarufu na maprodyusa wa filamu nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania, Maharage Chande akizungumza katika hafla hiyo.
 Uzinduzi huu ulilenga kwenye kusheherekea kazi nzito za maprodyusa wetu wa filamu hapa nyumbani , na utambulisho rasmi wa chaneli yetu yenye mandhui ya kitanzania. Chaneli hii imelenga kuburudisha na kuelimisha watazamaji wetu wa kitanzania kupitia filamu, tamthiliya, na maigizo mbalimbali ya Kiswahili. 
Mkurugenzi Mkuu wa MNET, Yalisa Phawe akizungumza. Kulia ni Mkuu wa Chaneli ya Maisha Magic Bongo, Barbara Kambogi.
 Chaneli hii inapatikana kwenye kifurushi cha huduma za DStv (160). Uzinduzi huo ulifuatiwa na maonesho ya tamthilia ya kimapenzi ya “Huba”, na vidokezo vya video za mambo yajayo yaliyoandaliwa kwenye chaneli ya Maisha Magic Bongo. Watazamaji wetu wajiandae kwa uhondo zaidi kupitia vipindi vijavyo vya “Harusi Yetu”, 
Mwenyekiti wa Bodi ya DSTV, Balozi Ami Mpungwe.
Movi za kihindi zenye tafsiri ya Kiswahili kama “Doli”, na filamu mbalimbali kuanzia msimo mpya wa Februari 2017.

Wakati wa mahojiano na waandishi wa habari, Mkuu wa chaneli ya Maisha Magic Bongo Barbara Kambogi alisema “Tumefurahia kupata fursa ya kuwapatia watazamaji wetu wa kitanzania chaneli ya Maisha Magic Bongo yenye mandhari halisi ya Kiswahili.

Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fisoo.
Tumebahatika kusheherekea maadhimisho yetu ya Maisha Magic Bongo kutimiza mwaka mmoja. Pamoja na hayo, tunatambua mchango mkubwa wa maprodyusa wa filamu za kitanzania katika kushirikiana nasi. 

Kwani kwa pamoja tumeweza kuiendeleza tasnia yetu ya kitanzania. Ndugu zangu, huu ni mwanzo tu wa Maisha Magic Bongo na tunatarajia kusonga mbele. Tutaendelea kushirikiana na maprodyusa wa filamu za hapa nyumbani, kwani sasa tumewapa fursa maprodyusa wetu kutusaidia kuitangaza sanaa yetu ya Tanzania kwenye masoko ya nje.”

Maisha Magic Bongo chaneli (160) imewaandaliwa mambo mazito na ya uhakika ili kuburudisha  wateja wetu  na kujivunia utanzania wetu kupitia kazi nzito za maprodusa na waigizaji wetu.

Mgeni rasmi alimalizia kwa kuishukuru Maisha Magic Bongo kwa kuisogeza mbele sanaa ya filamu ya Tanzania na kuendeleza vipaji vya maprodyusa wetu kupitia kazi zao nzuri.”

No comments:

Post a Comment