Tuesday 29 November 2016

Mjomba Mrisho Mpoto aendelea kuchengua Ikulu baada ya kupewa shavu katika dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa rais Lungu wa Zambia


 Rais Dk John Pombe Magufuli akimpongeza muimbaji mahiri wa mashairi, Mrisho Mpoto Ikulu jijini Dar es Salaam hivi karibuni wakati msanii huyo akiimba kibao cha Sizonje.

Na Mwandishi Wetu
MUIMBAJI mashuhuri wa mashairi nchini, Mrisho Mpoto ameendelea kupata shavu katika hafla mbalimbali zinazofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mpoto, juzi alitoa burudani kali Ikulu wakati wa dhifa ya kitaifa ambayo Rais John Magufuli alimuandalia mgeni wake Rais wa Zambia, Edgar Lungu.

Katika hafla hiyo, msanii huyo ambaye sasa anatamba na kibao chake cha Sizonje, aliimba wimbo unaosifu na kuelezea ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Zambia.

Wageni waalikwa walifurahia maneno yaliyomo katika wimbo huo, yakiwemo yale yaliyowaelezea waasisi wa mataifa hayo mawili, Julius Nyerere (Tanzania sasa ni marehemu) na Kenneth Kaunda wa Zambia.

Pia alielezea kuhusu Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), bomba la mafuta la Tazama, na mambo mengine mengi, ambayo yanaunganisha nchi hizi mbili.

Hivi karibuni Magufuli alitamka wazi kuwa yeye ndio Sizonje, ambaye nsiye anayezungumzia katika kibao hicho chenye mafumbo kibao.
Akiwa nchini, Rais Lungu mbali na kutembelea Tazara na Tazama, pia alitembelea baadhi ya vitengo vya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (PTA) kabla ya kuondoka jana kurudi kwao.

No comments:

Post a Comment