Saturday 26 November 2016

guardiola akiri michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya sio mchezo



MANCHESTER, England
KOCHA wa Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa kufanya kwake vizuri katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya haina maana kuwa ana uhakika wa kufanya vizuri katika mashindano hayo msimu huu.

Katika misimu saba kama kocha wa Barcelona na Bayern Munich, Guardiola mwenye umri wa miaka 45 ameshinda mara tatu taji la Ligi ya Mabingwa na hajawhi kushindwa kufuzu kwa nusu fainali.

Man City msimu huu imefikia hatua ya mtoano ya mashindano hayo huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi.

"Wakati wote inaonekana kama rahisi lakini kila kitu ni kigumu, alisema Guardiola.

Timu hiyo ya kocha huyo Mhispania itamaliza ya pili katika Kundi C, ikiwa na maana kuwa wataikwepa Bayern Desemba 12  wakati itakapopangwa ratiba ya hatua ya 16 bora.

Juventus na Borussia Dortmund ni wapinzani wanaotarajia kkutana pamoja na Monaco, ambao wamemaliza kileleni katika kundi ambalo Tottenham walitolewa katika mbio hizo.

Man City ilitinga hatua ya nusu fainali msimu uliopita, ambapo huku nyuma haijawahi kuvuka hatua ya 16 bora.

"Tunazungumza kuhusu Manchester City kucheza hatua ya nusu fainali lakini kuna timu nzuri kibao Ulaya, alisema Guardiola.

"Kucheza robo fainali sio jambo la kawaida. Wakati unapofanikiwa kucheza nusu fainali au fainali, ni kitu kisicho cha kawaida.

"Kiwango chetu sasa ni kucheza hatua ya mtoano kama ni kiwango chetu cvha chini, ndio miaka sita iliyopita hilo halikuwahi kutokea kamwe.

No comments:

Post a Comment