Monday 21 March 2016

Arsene Wenger alia na mashabiki wa Arsenal kumzomea licha ya kushinda



Kocha wa Arsenal, Mfaransa Arsene Wenger akiwasili kabla ya mchezo wa timu yake na ile ya Everton wa Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Goodison Park jijini Liverpool mwishoni mwa wiki.
LONDON, England
ARSENE Wenger anakiri kuwa ameachwa na `maumivu baada ya mashabiki wa Arsenal kutokuwa na imani naye katika mechi za hivi karibuni.

 Ushindi wa timu hiyo wa mabao 2-1 dhidi ya Leicester City mwezi Februari uliirejesha timu hiyo katika mbio za ubingwa, lakini vipigo kutoka kwa Manchester United na Swansea City na sare dhidi ya Tottenham viondoa matumaini kwa timu hiyo.

Kipigo cha jumla ya mabao 5-1 kutoka kwa Barcelona katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na kufungwa nyumbani kwa mabao 2-1 dhidi ya Watford katika Kombe la FA kumeifanya Arsenal kusalimisha nafasi yake ya kutwaa taji msimu huu.

Mashabiki wameongeza upinzani dhidi ya kocha huyo mkongwe katika Ligi Kuu ya England, ambapo wametaka atimuliwe ili timu hiyo ifanye vizuri.

Pia mashabii wamekuwa wakimlaumu mmoja wa wamiliki wenye hisa kubwa katika klabu hiyo, Stan Kroenke.

"Kitu kinachoniuma sana ni kwamba katika kipindi muhimu cha msimu ndio tunacheza katika mazingira magumu,  

alisema Wenger baada ya Arsenal kurejea katika mstari kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Everton Jumamosi.

Baada ya mchezo wa Tottenham ambako tulicheza mchezo mzuri sana, tulicheza na wachezaji 10 dhidi ya 11 na tulitoka nyuma na kutoka sare ya mabao 2-2, kwa kweli sielewi kwanini sasa wakati tunahitaji kila mmoja awe nyuma yetu, tunakuwa na mvurugano.

"Kutoka katika vyombo vya habari, sawa. Lakini hata kwa mashabiki wetu? Ni ngumu kulipokea hilo.

Kitu kizuri kwa Arsenal kwa sasa ni kiwango cha kuvutia cha Danny Welbeck, ambaye alifunga bao lake la nne katika mechi tisa tangu arejee uwanjani kutoka katika maumivu wakati alipofunga bao katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Goodison Park.

No comments:

Post a Comment