Tuesday 29 March 2016

Maandalizi Ngorongoro Marathon 2016 yapamba moto, Waziri Maghembe athibitisha kuzindua mbio hizo Aprili 16



Baadhi ya wanariadha wakichuana katika mbio za Ngorongoro Marathoni 2012 na mbio hizo zimeendelea kukuwa kila mwaka na kushirikisha washiriki kibao kutoka ndani na nje ya nchi.

  Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Jumanne Maghembe amethibitisha kuanzisha msimu wa tisa wa mbio za Ngorongoro Marathon zitakazofanyika Aprili 16.

Mmoja wa waratibu wa mbio hizo, John Mbando alisema kuwa, Maghembe amethibitisha kuwa mgeni rasmi wa mbio hizo za kila mwaka.
 
Mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania, Fabian Joseph akimaliza mbio za Ngorongoro Marathon 2012 kwenye Uwanja wa Mazingira Bora mjini Karatu
Mbio za mwaka huu zinatarajia kuwa na msisimko mkubwa na zitashirikisha zaidi ya wanariadha 2,000 kutoka nje na ndani ya Tanzania.

Mbando alisema kuwa mbio hizo zitaanzia katika lango kuu la kuingilia na kutokea katika Hifadhi ya Ngorongoro na kumalizia kwenye viwanja vya Mazingira Bora mjini Karatu mkoani Arusha.
Kampuni mbalimbali zimekuwa zikijitokeza kudhamini mbio hizo. Pichani Tigo walipodhamini mbio za mwaka 2013.
 Mbali na kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasomesha watoto wa kimaasai, pia mbio hizo zinasaidia kupiga vita ugonjwa hatari wa malaria kwa kuwaelimisha watu na kutoa vyandarua.

Mshindi wa kwanza katika mbio za kilometa 21 kwa upande wa wanawake na wanaume, kila mmoja ataondoka na sh. 2,000,000 huku mshindi wa pili ataondoka na sh. 1,000,000 na watatu sh. 500,000.

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akisalimiana na mmoja wa waratibu wa Ngorongoro Marathon 2013. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ambaye pia ni Rais wa Riadha Tanzania (RT) wakati huo Mtaka alikuwa mkuu wa wilaya ya Mvomero.
Zaidi ya sh. Milioni 6 zimetengwa kwa ajili ya zawadi za washindi, ambapo pia kutakuwa na mbio za kilomita tano na zile za wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za kilomita 2.5.

Mbio za mwaka huu zinadhaminiwa na Maji ya Kilimanjaro pamoja na Zara Tours na Zara Charity za zingine.
Kabla ya kuanza kwa mbio za Ngorongoro 2013 katika lango kuu la kuingilia na kutokea katika Hifadhi ya Ngorongoro

Nyalandu akimkabidhi zawadi mshindi wa mbio za Ngorongoro 2013 Dickson Marwa. Kushoto ni Alphonce Felix mshindi wa pili wa mbio hizo.
Wanariadha wakichuana katika mbio za Ngorongoro 2013.

No comments:

Post a Comment