Tuesday 29 March 2016

Wenger atamba kuendelea kuifundisha Arsenal msimu ujao, awaponda wanamkosoa na kutaka atimuliwe



Kocha Arsene Wenger.

LONDON, England
ARSENE Wenger anasema kuwa "hana wasiwasi" kuwa ataendelea kuifundisha Arsenal mwanzoni mwa msimu ujao.

Wenger amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake na kumekuwa na uvumi mkubwa kuhusu hatma ya kocha huyo Mfaransa katika klabu hiyo kufutia matokeo mabovu katika wiki za hivi karibuni.

Kimsimamo, Arsenal kwa sasa iko katika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu, pointi 11 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Leicester City.

Kikosi cha Wenger pia kilitupwa nje ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya pamoja nay ale ya Kombe la FA mwezi huu, matokeo yaliyosababisha baadhi ya mashabiki wa timu hiyo kuja juu.

Mashabiki hao wamechukulizwa na mwenendo mbovu wa timu hiyo,ambapo wamemtaka kocha huyo kuachia ngazi ili timu hiyo ipate mafanikio.

Hatahivyo, kocha huyo mwenye umri wa miaka 66, ambaye ameifudisha Arsenal kwa misimu 20, anasisitiza kuwa ana uhakika kwa asilimia 100 ataiwezesha timu hiyo kufanya vizuri msimu ujao.

Alipoulizwa kama ataendelea kuwa kocha wa Arsenal msimu ujao, Wenger alisema: "Sina wasiwasi kwasababu nimejitoa kuisaidia timu kufanya vizuri. Kama ninafanya kitu, nakifanya kwa asilimia 100. Wakati wote hujitoa kuiwezesha timu kufanya vizuri.

No comments:

Post a Comment