Friday, 27 October 2017
Fifa yaongeza zawadi Kombe la Dunia
ZURICH, Uswisi
MATAIFA 32 yatakayoshindana
katika fainali za Kombe la Dunia 2018 yatagawana kiasi cha dola za Marekani
milioni 400 (sawa na sh bilioni 898) katika zawadi ikiwa ni ongezeko la asiliia
12 ya fedha za mashindano ya mwaka 2014, Fifa imesema.
Katika taarifa
yake jana Shirikisho hilo la Kimataifa la Soka limesema kuwa fedha zawadi
katika mashindano yaliyopita yaliyofanyika Brazil zilikuwa dola za Marekani
milioni 358.
Imeelezwa kuwa
Ujerumani ambaye ni bingwa wa Kombe la Dunia alindoka na kitita cha dola za
Marekani milioni 35, huku mshindi wa pili Argentina alipata dola milioni 25.
Tofauti, nchi
ambazo zitashindwa kuvuka hatua ya makundi kila moja itapokea kiasi cha dola za
Marekani milioni 8.
Katika mkutano wa
Fifa uliofanyika Kolkata, bodi hiyo ya Fifa pia imepitisha taratribu za kuomba
uenyeji wa Kombe la Dunia kwa ajili ya mwaka 2026.
Huku ikithibitisha
tarehe za mashindano mbalimbali, yakiwemo ya Kombe la Dunia yatakayofanyika
Falme za Kiarabu na yale ya wanawake ya mwaka 2019 yatakayofanyika Ufaransa.
Fainali za Kombela
Dunia za mwaka 2018 zitafanyika kuanzia Desemba 12 hadi 22, wakati yale ya
wanawake ya mwaka 2019 yamepangwa kufanyika kuanzia Juni 7 huku fainali
ikifanyika Julai 7.
Wednesday, 25 October 2017
TB Three kutumia mitambo ya Visa ya Elektroniki
Na Mwandishi Wetu
JENGO la tatu la
abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII)
linalotarajiwa kukamilika Desemba 2018, litafungwa mfumo wa huduma ya viza kwa
njia ya mtandao (e-visa), ambao utarahisha na kuharakisha upatikanaji wake.
Kaimu Mkuu wa
Kitengo cha Uhamiaji cha JNIA, Bw. Kaanankira Mbise amemwambia jana Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano),
Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye alipotembelea eneo la uombeaji viza kwa abiria
wa kimataifa wanaowasili, kuwa wanatarajia kutumia huduma hiyo ambayo ni rahisi
na haraka.
“Tayari mkakati
umeanza wa kuanzisha huduma hii ya e-visa hivyo tukifanikiwa utafungwa katika
jengo hili jipya, ambapo itasaidia kwa abiria kuipata huduma hiyo kwa haraka
kwani itatumia mtandao,” amesema Bw.
Mbise.
Hata hivyo, Bw.
Mbise amesema kwa sasa wameboresha huduma hiyo kwa wasafiri wanaowasili katika
jengo la pili la abiria (JNIA-TBII) , ambapo tayari wamepatiwa mashine nne za
kisasa zinazosaidia kupunguza msongamano wa abiria wenye kuhitaji huduma hiyo,
hususan kipindi cha mchana chenye ujio wa ndege nyingi za nje ya nchi.
“Hizi mashine
zimeharakisha upatikanaji wa huduma kwani tumeweza kuhudumia abiria wengi kwa
wakati mmoja, na msongamano umepungua kiasi tofauti na awali mashine zilikuwa
chache.” amesema Mbise.
Naye Mhe. Mhandisi
Nditiye amesema baada ya ziara yake amegundua mashine za viza ni za muda mrefu
na zinahudumia abiria mmoja kwa mrefu, na tayari ameuagiza uongozi wa Mamlaka
ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kuwasilisha kwa maandishi mapendekezo yao
ya namna ya kuharakisha huduma hiyo, ili serikali iyafanyie kazi kwa kusaidia
kuondoa kero hiyo.
“Nimegundua kuna
baadhi ya mashine za viza zimeongezwa lakini pia zilizopo zimechoka kwani ni za
muda mrefu na zinahudumia abiria mmoja kwa muda mrefu na hii inaharibu sifa ya
kiwanja chetu kwa wageni wanaokuja hapa nchini,” amesema Mhandisi Nditiye.
Hata hivyo,
amesema wanampango wa kuongeza madirisha ya benki yanayolipia viza hizo ili
kuharakisha huduma hiyo, ambapo sasa ni machache kulinganisha na idadi kubwa ya
abiria wanaowasili kwa ndege kubwa. Ndege hizo ni Emirates, Etihad, Oman Air,
Qatar, South Africa Air na Ethiopia, ambazo zimekuwa zikipishana kwa muda
mfupi.
Naye Kaimu
Mkurugenzi wa TAA, Richard Mayongela amesema tayari wanampango wa kuongeza
upana wa eneo hilo la wasafiri wanaowasili wa kimataifa, ambapo sasa kumekuwa
na msongamano kutokana na ufinyu wake.
“Hili jengo
linazaidi ya miaka 30 na ukiangalia abiria waliokuwa wamekadiriwa wakati ule
lilikuwa likikidhi mahitaji, lakini sasa abiria wameongezeka na eneo limekuwa
dogo, hivyo tayari tumeanza kwa kuondoa baadhi ya ofisi ili kuongeza upana
wake, ninaimani litapunguza msongamano uliopo sasa,” amesema Bw.
Mayongela.
Lakini pia Bw.
Mayongela amesema sasa wapo katika mazungumzo na Mamlaka ya Usafiri wa Anga
(TCAA), ili kuangalia namna bora ya kuzipangia muda ndege zinazopishana muda
mdogo kwa wakati wa mchana ili ziachiane muda mrefu, ambapo kutasaidia
kupunguza msongamano
Awali eneo hilo
linakumbwa na changamoto kubwa ya msongamano wa abiria wanaohitaji huduma ya
viza baada ya uchache mashine zinazosimamiwa na Idara ya Uhamiaji zilizokuwepo
na kufanya abiria wanaohitaji huduma hiyo kutumia muda mrefu kuipata.
Tuesday, 24 October 2017
Chaneta walivyokabidhiana `ofisi' Uwanja wa Taifa
![]() |
Makamu mwenyekiti wazamani wa Chaneta, Zainabu Mbiro akipanda katika gari la Chama jhicho aina ya Noah wakati akilikabidhi kwa uongozi mpya wa Chaneta kwenye Uwanja wa Taifa. |
![]() |
Mwenyekiti Mpya wa Chaneta, Dk Devota Marwa akikagua garia aina ya Noah baada ya kukabidhia nyaraka mbalimbali na uongozi uliopita pamoja na gari hilo. |
Ronaldo, Zidane wang'ara tuzo za Fifa 2017
LONDON, England
CRISTIANO Ronaldo
ametangazwa kuwa ndiye mchezaji bora wa dunia wa kiume katika tuzo za
Shirikisho la Kimataifa la Soka 2017 zilizofanyika jijini hapa.
Mshambuliaji huyo
wa Real Madrid na Ureno aliwapiga kumbo mwenzake wa Barcelona Lionel Messi na
yule wa Paris St-Germain, Neymar katika mbio za kutwaa tuzo hiyo.
Ronaldo, 32,
aliisaidia Real Madrid kutwaa mataji mawili, likiwa lile le La Liga, ambalo
walilitetea na La Liga msimu wa mwaka 2016-17.
Lieke Martens wa
Barcelona na Uholanzi alishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia wakike, huku
kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane alitangazwa kuwa kocha bora wakiume na
Mholanzi Sarina Wiegman amekuwa kocha bora wakike.
Mchezaji wa
Arsenal Olivier Giroud alipokea tuzo ya Puskas kwa ajili ya bao lake bora 2017
walipocheza dhidi ya Crystal Palace Januari.
Tofauti ya Ballon
d'Or na Fifa?
Hii ni mara ya pili
kufanyika tuzo hizo za Fifa za soka, ambazo ni tofauti na zile za Ballon d'Or.
Tuzo ya Ballon
d'Or ilikuwa ikitolewa na jarida la Soka la Ufaransa tangu mwaka 1956, lakini
Fifa ilijitenga na tuzo hizo na kuanzisha zake.
Badala yake,
ilianzisha tuzo za tuzo za mchezaji bora wa Fifa, ambapo Ronaldo ndiye alikuwa
mchezaji wa kwanza kutwaa tuzo hiyo Januari.
Kura za kumpata
mchezaji na kocha bora zinapigwa na manahodha wa timu za taifa na makocha,
waandishi wa habari walioteuliwa, na kwa mara ya kwanza, kura za katika mtandao
zilipigwa na mashabiki. Kila kundi lilikuwa na asilimia 25 ya kura.
Cristiano Ronaldo
Ni mwaka mwingine
wa kuvutia kwa Ronaldo, ambaye aliyetwaa tuzo ya kwanza ya mchezaji bora wa
Fifa wa Dunia baada ya kuiongoza Ureno kutwaa taji la Euro 2016.
Mwaka huu alifunga
mabao mawili wakati Real Madrid ikishinda 4-1 dhidi ya Juventus katika fainali
ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na pia alizifumania nyavu mara 25 katika mechi 29
alizoichezea klabu yake katika La Liga ikiwa ni kwa mara ya kwanza katika miaka
mitano.
"Tuko England
kwa mara ya kwanza, na tumeshinda kwa mara ya pili mfululizo. Huu ni wakati
mzuri kwangu, “alisema Ronaldo alipokuwa akizungumza wakati wa kukabidhiwa tuzo
hiyo.
Wachezaji watatu
wakiume
Cristiano Ronaldo
- 43.16 % Lionel Messi - 19.25 % Neymar - 6.97%
Messi alimpigia
kura mchezaji mwenzake wa Barcelona Luis Suarez kama mchezaji bora, wakati
Ronaldo naye pia alimpigia mchezaji mwenzake wa Real, Luka Modric.
Kocha wa England
Gareth Southgate alimpigia kura Ronaldo.
Mchezaji bora
wakike
Martens, 24,
alikuwa mhimili wa timu ya taifa ya Uholanzi katika ushindi wa timu hiyo katika
mashindano ya Mataifa ya Ulaya, ambapo alishinda tuzo ya mashindano hayo.
Fifpro World XI
Fifa imefanya
mabadiliko matatu katika kikosi cha mwaka 2016. Kipa Gianluigi Buffon
alimbadili Manuel Neuer, wakati mchezaji wa AC Milan Leonardo Bonucci
alimbadili mchezaji wa Barcelona, Gerard Pique katika nafasi ya beki bora na
mchezaji wa PSG Neymar ameshika nafasi ya ushambuliaji bora hiyo badala ya Luis
Suarez.
Orodha ya
wachezaji hao watano ni kutoka Real Madrid, wawili Barcelona, wawili PSG, mmoja
Juventus na mmoja AC Milan. Hakuna mchezaji wa Ligi Kuu ya England aliyomo
katika kikosi hicho.
Kocha bora
Real ilimaliza
msimu uliopita ikiwa bingwa wa Hispanuia na kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2012
na kutwaa ubigwa wa Ulaya kwa mara ya pili mfululizo.
Zidane alishinda
tuzo hiyo akimshinda kcha wa Chelsea Antonio Conte, ambaye alitwaa taji la Ligi
Kuu katika msimu wake wa kwanza England, na yule wa Juventus, Massimiliano
Allegri, aliyeiongoza timu yake kutwaa mataji mawili ya Serie A na lile la
Coppa Italia.
Makocha watatu wakiume
Zinedine Zidane -
46.22% Antonio Conte - 11.62% Massimiliano Allegri - 8.78%
Kocha bora wakike
Mholanzi Wiegman
alioongoza timu yao ya taifa kutwaa taji la Euro 2017 katika ardhi ya nyumbani,
ambapo timu hiyo ilicheza soka safi la kuvutia.
Hilo lilikuwa taji
lao la kwanza kubwa la kimataifa kwa timu ya wanawake baada yakuifunga Denmark
katika fainali.
Tuzo ya Puskas
Bao bora la mwaka
2017 ni lile lililofungwa na mchezaji wa Arsenal, Giroud.
Bao hilo
lilifungwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Palace siku ya mwaka
mpya, ambapo mshambuliaji huyo Mfaransa alifunga bao safi aliunganisha krosi ya
Alexis Sanchez niliyopigwa nyuma yake.
Kipa bora
Bingwa wa Kombela
Dunia, na mshindi mara 10 wa taji la Serie A, Gianluigi Buffon ndiye mshindi wa
kwanza wa tuzo ya kipa bora.
Kipa huyo mkongwe
aliisaidia Juventus kutwaa mara sita mfululizo taji la Serie A na kucheza
dakika 600 bila kuruhus bao katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.
Buffon, 39, alitwaa
tuzo hiyo akiwashinda Keylor Navas, Manuel Neuer, aliyeisaidia Bayern Munich
kutwaa Bundesliga.
Naibu Waziri aridhishwa na Ujenzi Terminal Three
Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye amesema kuwa ameridhika na
maendeleo ya ujenzi wa sehemu ya tatu (Terminal III) ya Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Nditiye ambaye
yuko upande wa sekta ya Uchukuzi na Mawasiliani aliyasema hayo leo baada ya
kutembelea sehemu zote za JNIA kuanzia Terminal One hadi Three na kujionea
mambo mbalimbali.
Amesema kuwa
ameridhishwa jinsi ujenzi huo unavyoendelea, ambao unatarajia kukamilika
Septemba mwakani.
Alimtaka
mkandarasi, ambaye ni Kampuni ya BAM International kuendelea na kazi bila
kusita, kwani Serikali imeshatoa fedha za ujenzi huo.
Amesema kuwa pia
amefurahishwa na mipango ya biashara baada ya kumalizika kwa kiwanja hicho,
ambapo kutakuwa na migahawa, mahoteli jirani na sehemu hiyo ya Terminal Three.
Amesema amegundua
changamoto ndogo ndogo kama suala la mpango wa biashara kuwepo na mahoteli
kuzungunguka eneo hilo, ambapo tayari amewaagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
(TAA) kushughulikia hilo.
Kingine ni
uchakavu wa mashine za kupozea hewa na mashine za viza kutumia muda mrefu katika Terminal Two,
mfano viza ya Ujerumani inakuwa ngumu kushughulikiwa na mashine hizo.
Pia alitaka
mlolongo mrefu wa malipo katika benki ya NMB pale kiwanjani cha JNIA Terminal Two
kutatuliwa haraka ili kuwapunguzia muda wasafiri.
Mkandarasi anataka
kufanya vitu vya ziada na tayari wameshaelekezana naye na atavifanya, kwani
viko ndani ya mkataba.
Amesema mikataba
mipya katika eneo hilo la Terminal Three litakapokamilika, kipaumbele watapewa
wafanyabiashara wazalendo, lakni wale wasafi wasiokuwa wababaishaji.
Huduma kwa
abiria itakuwa bora zaidi kuliko kule kwa sababu eneo hilio ni la kisasa zaidi.
Amesema
anaishukuru Serikali kwa kuisaidia TAA katika shughuli mbalimbali kama
alivyoahidi Naibu Waziri.
"Kupitia Wizara, huduma mbalimbali zitaboreshwa kama alivyosema Naibu Waziri tupeleke
bajeti yetu ili waweze kutusaidia, "amesema.
Kaimu Mkurugenzi
wa JNIA, Johannes Munanka amesema kuwa kutakuwa na programu maalum ya
kuutangaza uwanja huo kwa wananchi, ambapo aliwataka kuutembelea ili kuona
shughuli zake na kujifunza mambo mbalimbali.
NAIBU Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye amesema kuwa ameridhika na
maendeleo ya ujenzi wa sehemu ya tatu (Terminal III) ya Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Nditiye ambaye
yuko upande wa sekta ya Uchukuzi na Mawasiliani aliyasema hayo leo baada ya
kutembelea sehemu zote za JNIA kuanzia Terminal One hadi Three na kujionea
mambo mbalimbali.
Amesema kuwa
ameridhishwa jinsi ujenzi huo unavyoendelea, ambao unatarajia kukamilika
Septemba mwakani.
Amesema kuwa ujenzi unaendelea vizuri tena kwa kasi kubwa licha ya kuwepo kwa baadhi ya changamoto katika mradi huo, ambazo zinafanyiwa kazi.
Alimtaka
mkandarasi, ambaye ni Kampuni ya BAM International kuendelea na kazi bila
kusita, kwani Serikali imeshatoa fedha za ujenzi huo.
Amesema kuwa pia
amefurahishwa na mipango ya biashara baada ya kumalizika kwa kiwanja hicho,
ambapo kutakuwa na migahawa, mahoteli jirani na sehemu hiyo ya Terminal Three.
Amesema amegundua
changamoto ndogo ndogo kama suala la mpango wa biashara kuwepo na mahoteli
kuzungunguka eneo hilo, ambapo tayari amewaagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
(TAA) kushughulikia hilo.
Kingine ni
uchakavu wa mashine za kupozea hewa na mashine za viza kutumia muda mrefu katika Terminal Two,
mfano viza ya Ujerumani inakuwa ngumu kushughulikiwa na mashine hizo.
Pia alitaka
mlolongo mrefu wa malipo katika benki ya NMB pale kiwanjani cha JNIA Terminal Two
kutatuliwa haraka ili kuwapunguzia muda wasafiri.
Mkandarasi anataka
kufanya vitu vya ziada na tayari wameshaelekezana naye na atavifanya, kwani
viko ndani ya mkataba.
Amesema mikataba
mipya katika eneo hilo la Terminal Three litakapokamilika, kipaumbele watapewa
wafanyabiashara wazalendo, lakni wale wasafi wasiokuwa wababaishaji.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela amesema kuwa sehemu hiyo ya Termila Three itakapokamilika itahudumia Abiria milioni 6 kwa mwaka, ambao watakuwa wakihudumiwa kwa haraka na kwa nafasi na kuwepo sehemu bora ya kufanya biashara kuliko Terminal Two.
Huduma kwa
abiria itakuwa bora zaidi kuliko kule kwa sababu eneo hilio ni la kisasa zaidi.
"Kutokana na huduma bora na ukubwa wa eneo tunatarajia kupata abiria wengi zaidi, "amesema.
Alisema kuwa jengo chakavu la Terminal Two litafanyiwa ukarabati ili kuwa la kisasa, ambapo mifumo mbalimbali itaboreshwa ili kuwahudumia abiria kwa haraka zaidi.
Amesema
anaishukuru Serikali kwa kuisaidia TAA katika shughuli mbalimbali kama
alivyoahidi Naibu Waziri.
"Kupitia Wizara, huduma mbalimbali zitaboreshwa kama alivyosema Naibu Waziri tupeleke
bajeti yetu ili waweze kutusaidia, "amesema.
Kaimu Mkurugenzi
wa JNIA, Johannes Munanka amesema kuwa kutakuwa na programu maalum ya
kuutangaza uwanja huo kwa wananchi, ambapo aliwataka kuutembelea ili kuona
shughuli zake na kujifunza mambo mbalimbali.
Monday, 23 October 2017
Kozi ya awali ya mafunzo ya Anga yafunguliwa leo
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA), (wa pili kushoto waliokaa), Johannes Mnaka, mkuu wa chuo cha Anga, Enirisha John (katikati waliokaa). Kushoto waliokaa mkufunzi Thmarat Abeid, Kulia waliokaa mkufunzi na wa pili kulia ni Fatuma Makimba, ambaye ni Meneja Rasilimali Watu wa JNIA, akiwa pamoja na viongozi wengine na wanafunzi wa kozi ya awali ya Anga leo jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa kozi ya awali ya Anga wakati wa ufunguzi wa kozi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA), Johannes Mnaka akifungua kozi ya awali ya anga katika Chuo cha Anga jijini Dar es Salaam mapema leo.
Wanafunzi wa kozi ya awali ya Anga wakati wa ufunguzi wa kozi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA), Johannes Mnaka akifungua kozi ya awali ya anga katika Chuo cha Anga jijini Dar es Salaam mapema leo.
Lulu akana kusababisha kifo cha Steven Kanumba
Na Mwandishi Wetu
MUIGIZAJI wa
Filamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam kuwa hakusababisha kifo cha mpenzi wake Steven Kanumba na badala yake
yeye ndiye angeuawa baada ya kupigwa na panga.
Lulu ambaye
amebainisha wazi kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi kwa miezi minne na
Kanumba, alikuwa akienda mara kwa mara nyumbani kwake na kwamba walikuwa
wanaficha mahusiano yao ili kukwepa mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.
Akiongozwa na
Wakili wake, Peter Kibatala, Lulu alidai mbele ya Jaji Sam Rumanyika kuwa Aprili 6, 2012
alikuwa nyumbani kwao Tabata na jioni alitaka kwenda kwa marafiki zake
Mikocheni kwa ajili ya kwenda klabu.
Alidai walikuwa
wakiwasiliana na marehemu Kanumba kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi licha
ya kwamba hakutaka kumwambia kama anataka kutoka na marafiki zake kwa sababu
alikuwa hapendi atoke.
"Marehemu
alikuwa akinipigia simu mara nyingi kujua nipo wapi ndipo nilimwambia kuwa
nataka kutoka ili asinisumbue nikamueleza kuwa nitapita nyumbani kwake kumuaga,
lakini sitokaa sana. Kabla ya kufika alinipigia na kunambia kuwa ataacha mlango
wazi hivyo nipite mpaka chumbani..nyumba niliizoea hata asipokuwepo nilikuwa
naenda," alidai Lulu.
Aliendelea kudai
kuwa alimkuta Kanumba chumbani akiwa na taulo huku akipaka mafuta kichwani,
ambapo yeye alikaa kitandani na kusalimiana.
"Kama
tunavyojua marehemu alikuwa anajipenda sana hivyo alikuwa ameweka superblack
kwenye nywele zake na kwamba alikuwa na mafuta maalum ili zing'ae.
Tulisalimiana na muda kidogo simu yake iliita na alipokea alikuwa ni Chaz
Baba akamwambia anakuja. Wakati huo
alikuwa anakunywa pombe aina ya Jack Daniel na Sprite na ameshaanza
kulewa," alidai.
Pia alieleza kwa
kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi atoke, alimtaka waende sehemu moja ambapo
mara nyingi akilewa huwa anampiga hivyo
hakutaka kumbishia kutoka naye.
Lulu alidai
hupendelea kwenda disco wakati marehemu Kanumba alikuwa anapenda kwenda kwenye
bendi ambazo alidai kwake ni za kizee
wakati huo aliwaahidi marafiki zake kuwa atarudi.
Alidai baadae
marafiki zake walianza kumpigia kumuuliza ulipo ambapo aliogopa kupokea simu
mbele ya Kanumba kukwepa kuulizwa
anakwenda wapi, hivyo alimuaga na kumueleza kuwa anakwenda kuchukua maji
jikoni na alipofika kwenye korido
Kanumba alimfuatilia kwa nyuma na kumuuliza anaongea na nani.
"Nilijua
utani huku nikiwa nacheka nikamjibu kuwa naongea na rafiki yangu kwa sababu
nilizoea anapenda kujua naongea na nani
lakini baadae nilianza kuogopa baada ya kuona sura yake imebadilika
hivyo nikawa natoka nje naye alianza kunifuata na hii sio mara ya kwanza
kunipiga na hufanya hivi akiwa amelewa maana hata mtu alinipigia au kumkumbatia
alikuwa hapendi," alieleza na kuongeza;
"Nilikimbia
hadi nje wakati huo marehemu alikuwa na taulo hivyo nikadhani kwamba ataona
aibu kutoka nje hivyo huku akiwa kifua wazi lakini alinifuata hadi nje umbali
wa hatua 28 lakini aliendelea kunikimbiza hadi getini akatoka nje ya geti
ambapo kuna barabara ya Sinza Kijiweni na Tandale..tuliendelea kukimbizana hadi
nikajificha lakini aliniona na kunipiga vibao na kunifunga mikono yangu kwa
mkono wake mmoja."
Muigizaji huyo pia
alidai Kanumba alianza kumpiga mateke na kumburuza huku akiwa na taulo lake na
kwamba mdogo wake, Seth Bosco alikuwepo lakini hakutoka kumsaidia.
Alidai baada ya
kuburuzwa alinyanyuka na alipelekwa moja kwa moja hadi chumbani na mlango
ulifungwa kwa funguo kwa ndani na kutupwa kitandani kwa sababu alihisi simu
aliyokuwa anaongea naye ni mwanaume mwingine.
Lulu alidai
marehemu Kanumba alitoa panga na kwa sababu walikimbia alikuwa anahema sana na
kumwambia kuwa atamuua hivyo alianza kumpiga kwa mabapa ya panga kwenye mapaja
naye alikuwa akikinga asikatwe usoni.
Vile vile,
alidai Kanumba alikuwa anapumua kwa kasi
na kutupa panga chini na kuwa kama mtu anayekabwa baadae alinguka na kujigonga
kwenye ukuta muda huo yeye alikuwa kitandani.
"Alipokuwa
anataka kuamka nilihisi anataka kunifuata tena nikitoka nikajifungia chooni
wakati huo yeye alianza kutapatapa.
Nilijaribu kupiga kelele kupata msaada lakini hakuna, baadaye nilisikia
kishindo cha mtu kuanguka au mlango uliobamizwa na kusikia ukimya.
Sikujuwa za kama
ameanguka nilihisi hasira zake tu kwani nilipofungua mlango wa bafuni nilimkuta amelala na wakati huo
kulikuwa na mwanga wa mshumaa kwani umeme ulikatika," alidai.
Lulu alidai kwa
akili zake aliwaza kuwa Kanumba alijifanyisha kuzimia ili isiwe tatizo kwake
ambapo alianza kumwambia kuwa hata mtu akija atamwambia kila kitu kilichotokea
lakini akawa hajibiwi.
Alidai alichukua
maji chooni na kumgusisha machoni kuona kama ataamka na baadaye alifungua
mlango na kumuita Seth na kumueleza kuwa Kanumba ameanguka ambaye naye
alijaribu kumuamsha lakini hakuamka na kumpigia simu daktari wake.
Lulu anasimulia
kuwa alimwambia Seth hawezi kubaki nyumbani hapo badala yake akitoa naye
atatoka kwani akiamka atamuua hivyo
aliondoka na gari hadi Coco Beach.
Aliendelea kudai
kuwa alimpigia simu daktari wa familia Paplas
ambaye alikuwa anajua mahusiano yao na wakati akiumwa alikuwa anamtibu
na kwamba alimueleza kuwa rafiki yake amempiga sana na iwe mara ya mwisho
kumtafuta kwa sababu alimshikia panga na siku nyingine atamuua.
Alieleza kuwa
alikuwa haruhusiwi kutoka nyumbani kwao usiku hivyo alikuwa anabeba nguo za
ziada na anaporudi nyumbani asubuhi hudanganya kama alitoka kuosha vyombo
wakati anatokea klabu.
"Nilipokea
simu nyingi kuniuliza kama kweli Kanumba amekufa nilimpigia simu Seth, ambapo
alikuwa hapokei nilimpigia Dk Paplas nikamuuliza kuhusu masuala ya nyumbani
imekuwaje kwa sababu amepigiwa simu kuuliza naye akamwambia kuwa hajafa ila
wapo hospitali na kukata simu. Baadaye Dk Paplas alinipigia kuniuliza niko wapi
tukutane," alidai
"Kwa sababu
nilijua Kanumba na huyu daktari ni marafiki, nilijua anamtumia rafiki yake
waweze kukutana tena mara ya kwanza
nilimkatalia na nikamuuliza kama amezidiwa yupo hospitali gani niende. Nilitaka
anihakikishie alipo na asije na Kanumba na wala hakunambia kama
ameshakufa," alieleza Lulu.
Alidai walikutana
Bamaga na Dk Paplas na ndipo askari walimkamata bila ya kumwambia sababu na
walipofika Kituo cha Polisi, Oysterbay Polisi akakutana na watu wengi akiwemo
msanii Vincent Kigosi 'Ray' na kuhisi kwamba Kanumba amekamatwa.
Alidai
alichukuliwa maelezo na kuonesha sehemu alizojeruhiwa kwa kipigo na askari wa
kike ndiye aliyethibitisha na kwamba alichukuliwa maelezo mara nne ambapo
alipata taarifa za kifo cha Kanumba akiwa selo.
Siku inayofuata,
Lulu alidai alimueleza Afande Ernatus kwamba anaumwa hivyo alipelekwa hospitali
ya Mwananyamala akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi na kuandikiwa dawa.
"Sijasababisha
kifo chake yeye ndiyo alikuwa ananishambulia kwa silaha pengine asingeanguka
mimi ndio ningekuwa marehemu kwa sababu sikuwa na njia yoyote ya kujitetea kwa
sababu ya umbile langu dogo," alidai Lulu.
Hata hivyo, Jaji
Rumanyika alimtaka Lulu kueleza kama wakati huo anaendesha gari alikuwa na
leseni, ambapo alidai kuwa hakuwa nayo mpaka baada ya matatizo hayo ndio
aliomba leseni.
Kesi hiyo
imeahirishwa mpaka leo ambapo upande wa utetezi utakuwa na shahidi mmoja
Josephine Mushumbus ambaye wanadai kuwa yupo nje ya nchi.
TFF yatangaza kuziona Yanga, Simba ni sh 10,000
Na Mwandishi Wetu
SHIRIKISHO la Soka
Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa mahasimu wa jadi, Simba na
Yanga utakaochezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Uhuru kuwa ni sh. 10,000 majukwaa
ya mzunguko wakati jukwaa kuu ni sh. 20,000.
Ofisa Habari wa
TFF, Alfred Lucas alisema jana kuwa utaratibu maalum umewekwa kuhakikisha idadi
inayotakiwa ya watu 22,000 ndiyo wanaoingia uwanjani.
Alisema mchezo huo utachezwa kwenye Uwanja wa Uhuru,
kwa kuwa uwanja mkubwa wa Taifa upo kwenye ukarabati.
Katika hatua
nyingine, Lucas alisema Kamati mpya ya Uongozi wa Bodi ya Ligi (TPLB) ya TFF
itafanya kikao chake cha kwanza mjini Dar es Salaam, Alhamis ya wiki hii na
kubwa likiwa ni maandalizi ya mchezo huo.
Alisema ajenda nyingine katika kikao hicho ni kuteua
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi na Kamati nyingine mbalimbali.
Hiyo ni baada ya
uchaguzi wa TPLB uliofanyika Jumapili Oktoba 15 mwaka huu na kupata uongozi
mpya chini ya mwenyekiti wake Clement Sanga na makamu wake Shani Mlingo.
Wajumbe ni Hamisi Madaki, Ramadhani Mahano, Almasi Kasongo na Edgar Chibura.
Neymar atolewa wakati PSG ikitoka sare
![]() |
Neymar akioneshwa kadi nyekundu wakati PSG ilipocheza dhidi ya Olympique de Marseille. |
PARIS, Ufaransa
NEYMAR alitolewa
nje kabla ya mchezaji mwenzake Edinson Cavani akithibitisha thamani yake kwa
mara nyigine tena kwa kufunga bao la kusawazisha katika dakika za mwisho wakati
Paris St Germain (PSG) ikitoka sare ya 2-2 dhidi ya wapinzani wao wakubwa
Olympique de Marseille.
Mshambuliaji huyo
wa Uruguay alisawazisha dakika moja ndani ya muda wa nyongeza kwa shuti kali la
umbali wa kama meta 20 baada ya Neymar kutolewa nje katika dakika ya 87 kwa
kadi ya pili ya njano.
Neymar ndiye
alikuwa wa kwanza kuipatia timu yake bao la kusawazisha katika dakika ya 33
kufuatia lile la kuongoza la Olympique de Marseille lililofungwa na Luiz
Gustavo katika dakika ya 16.
Awali, Marseille
walifunga bao la pili katika dakika ya 78 lililowekwa kimiani na Thauvin,
ambalo baadae PSG walisawazisha kupitia kwa Cavan na kunusurika kupata kipigo
cha kwanza.
Kimsimamo, PSG ina
pointi 26 baada ya kucheza mechi 10 ikiwa kileleni pointi nne zaidi ya Monaco
iliyopo katika nafasi ya pili.
"Ni bao
muhimu kwani mchezo ni kama ulikuwa umemalizika, lakini angalau tumeondoka na
pointi, “alisema Cavani.
Monaco wako nafasi
ya pili, pointi nne nyuma wakiwa na pointi 22 baadaya kuifunga Caen 2-0
Jumamosi.
Real Madrid yaifukuza Barcelona kimya kimya
MADRID, Hispania
MABINGWA watetezi
wa La Liga Real Madrid imefanya kweli baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0
dhidi ya Eibar na kupunguza tofauti ya pointi na vinara Barcelona, huku Karim
Benzema akianzia benchi.
Marco Asensio
aliing’arisha Real Madrid baada ya kufunga mabao mawili na kuiwezesha timu yake
hiyo kuibuka na ushindi huo.
Kwa ushindi huo,
Real Madrid sasa imepunguza tofauti ya pointi na Barcelona hadi kufikia tano
katika mbio hizo za kusaka ubingwa.
Mshambuliaji huyo
alilazimisha bao la kujifunga na kufunga la pili wakati Madrid ikipanda hadi
katika nafasi ya pili ikifikisha pointi 20, moja nyuma ya Valencia na moja
mbele ya Atletico Madrid, ambayo iliifunga Celta Vigo 1-0 ugenini.
Bao hilo pekee
lililoipatia ushindi Atletico Madrid liliwekwa kimiani na Kevin Gameiro.
Barcelona wenyewe
waliwafunga Malaga 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wao wa Nou Camp
Jumamosi wakati Valencia ilipoisambaratisha Sevilla 4-0.
Paulo Oliveira
aliijaza katika wavu wao krosi ya Asensio katika dakika ya 18, kabla
mshambuliaji huyo hajawafungia wenyeji bao la pili dakika 10 baadae kufuatia
mpira wa Isco.
Mchezaji
aliyeingia akitokea benchi Marcelo aliongeza la tatu katika dakika 82.
Zinedine Zidane
alifanya mabadiliko matano kutoka katika kikosi chake, ambacho kilitoka sare ya
1-1 nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa
Ulaya Jumanne iliyopita.
SuperSport uso kwa uso na TP Mazembe Shirikisho
![]() |
Kikosi cha mabingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika,TP Mazembe |
JOHANNESBURG,
Afrika Kusini
TIMU ya SuperSport
United ilikuwa imekamilika karibu katika kila idara wakati ikifuzu kwa fainali
ya Kombe la Shirikisho 2017 baada ya kushinda mabao 3-1 dhidi ya Club African.
Kwa ushindi huo,
SuperSport ya Afrika Kusini imetinga fainali kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya
mchezo huo wa nusu fainali ya pili uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade Olympique
Radès Jumapili.
Mchezo wa kwanza
wa nusu fainali ulifanyikia kwenye Uwanja wa Lucas Moripe, ambao ulimalizika
kwa sare ya kufungana bao 1-1.
Kwa matokeo hayo,
SuperSport itakutana na bingwa mtetezi TP Mazembe, ambayo iliifunga FUS Rabat
ya Morocco, katika fainali ya mechi mbili za nyumbani na ugenini mwezi ujao.
![]() |
Wachezaji wa SuperSports United. |
Bradley Grobler
aliwafungia wageni, huku Jeremy Brockie naye pia alizifumania nyavu wakati
Saber Khalifa aliwafungia wenyeji bao la kufutia machozi.
Al Ahly yaichapa Etoile sasa kucheza fainali Ligi ya Mabingwa wa Afrika 2017 na Wydad Casablanca
CAIRO, Misri
KLABU ya Misri ya
Al Ahly (pichani) sasa itakutana na Wydad Casablanca ya Morocco katika fainali ya mwaka
huu ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika baada ya kuichapa Etoile
du Sahel ya Tunisia kwa mabao 6-2.
Kwa ushindi huo,
Al Ahly imetinga fainali baada ya kupata ushindi wa jumla wa mabao 7-4 katika
mechi mbili za nusu fainali.
Katika mchezo wa
marudio wa nusu fainali uliofanyika jijini Alexandria, Al Ahly ilionekana
kuizidi kabisa safu ya ulinzi ya wapinzani wao hao wa Tunisia wakati wakikata
tiketi hiyo ya kucheza fainali ikiwa ni mara yao ya 11.
Baada ya Ali
Maaloul kufunga bao la kwanza kwa wenyeji dakika mbili baada ya kuanza mchezo
huo, Walid Azarou alifunga bao la pili na kuifanya Etoile kutoka kabisa nje ya
mchezo.
Bao la kujifunga
lililofungwa na Rami Rabiaa liliipeleka Al Ahly katika fainali ya kwanza tangu
mwaka 2013, huku Etoile ikijibu kupitia kwa Rami El Bedwi na Ihab Msakni kwa
maba waliyofunga baadae.
Miaka minne
iliyopita, Al Ahly iliifunga timu ya Afrika Kusini ya Orlando Pirates katika
fainali wakati walipofanikiwa kutetea taji lao waliloshinda miezi 12
iliyotangulia.
Mchezo huo wa
Jumapili ulipigwa mbele ya karibu mashabiki 40,000 jijini Alexandria, ambao
walisaidia kuiongezea nguvu Al Ahly baada ya mechi nyingi za Misri kuchezwa
bila ya mashabiki kutokana na sababu za kiusalama.
Kikosi cha kocha
Hossam El Badry sasa kitakutana na Wydad katika mechi mbili za fainali, baada
ya Wamorocco hao kuwafunga USM Alger ya Algeria kwa mabao 3-1 katia mchezo
uliofanyika Jumamosi.
Wakati huohuo,
Ahly sasa wanaweza kuongeza rekodi yao ya kutwaa taji hilo mara nane na hadi
kufikia mara tisa endapo watafanikiwa kuifunga Wydad.
Mchezo wa kwanza
wa fainali utafanyika wikiendi ijayo huku ule wa marudiano unatarajia kufanyika
Novemba 3-5.
Timu yoyote
itakayoshinda italiwakilisha bara la Afrika katika mashindano ya Fifa ya Kombe
la Dunia kwa klabu yatakayofanyika Japan Desemba.
Mkurugenzi TAA ataka Tughe kutetea wafanyakazi
Na Mwandishi Wetu
KAIMU Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela
amewataka viongozi wa Chama cha Wafanyakazi kusikiliza malalamiko
ya wafanyakazi
bila kubagua.
Bw.Mayongela
alisema viongozi wa Wafanyakazi kupitia matawi mawili ya Chama cha Wafanyakazi,
TAA Makao Makuu na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA),
kutenda haki kwa kusikiliza malalamiko ya wafanyakazi wote na kuyawasilisha kwa
wasilisha kwa mwajiri ili yafanyiwe kazi.
Alitoa kauli hiyo
juzi wakati viongozi wa matawi hayo walipokwenda kujitambulisha ofisi kwake TAA
Makao Makuu, ambapo alisisitiza kuwa wafanyakazi wa chini ndio wenye matatizo
makubwa, lakini hawasikilizwi na kutatuliwa matatizo yao kwa wakati.
“Ninashukuru
uongozi mmekuja kuonana nami, ninahitaji ushirikiano wenu kama Chama cha
Wafanyakazi, muwatumikie wafanyakazi kwa kutenda haki mkisikiliza matatizo ya
kila mmoja na kufikisha sehemu husika na ninawaahidi kuwa nanyi bega kwa bega
kutatua matatizo ya wafanyakazi kwani wao ndio wanafanya TAA iwepo, “alisema
Mayongela.
Alisema
wafanyakazi endapo wakifanya kazi bila manung’uniko wala makundi, mamlaka
itasonga mbele kwa kuwa na uongozi sio kupigana vita bali unatakiwa kujijenga
na kuwa kitu kimoja.
Hatahivyo alisema
kwa sasa yupo mbioni kuangalia namna ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi kwa kupitia makusanyo yatakayotokana na
vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuongeza tija na ufanisi wa kazi ili kuongeza
ari kwa wafanyakazi.
Aliendelea kusema
kuwa inaonekana wafanyakazi wengi wa TAA wamekata tamaa kutokana na kufanya kazi
nyingi na wakati mwingine kupitiliza muda wa kazi wa kawaida bila kupata
stahiki yeyote.
“Kwa msaada wa
Mungu nina imani atanionyesha wapi fedha zilipo na jinsi ya kuzitumia ipasavyo
kwa masuala ya msingi, na ninakusudia hadi kufika Desemba mwaka huu niweze
kuboresha maslahi ya wafanyakazi.
Watu wanafanya
kazi sana lakini maslahi ni madogo, unaona kabisa jinsi mtu anavyoitumikia
taasisi kwa moyo, lakini sura inaonesha jinsi alivyokata tamaa, ninaamini kwa
kufanya hivi itaongeza tija na bidii ya kazi.” Alisema Bw. Mayongela.
Halikadhalika, Bw.
Mayongela amesema atahakikisha wafanyakazi wanapata vitendea kazi vya uhakika
kulingana na kazi zao, zikiwemo bajaji, pikipiki na magari kwa ajili ya doria
na shughuli za uendeshaji ndani ya Viwanja vya Ndege.
Pia amewataka
viongozi hao kuwa karibu na wafanyakazi ili kuhakikisha wanawahamasisha
wanafanya kazi kwa bidii, uaminifu na uadilifu ili kuondoa mianya na tabia za
upokeaji wa rushwa, kwa kuwa TUGHE ni daraja kati ya mwajiri na wafanyakazi.
Naye Mwenyekiti wa
TUGHE tawi la TAA Makao Makuu, Bw. Nasib Elias mbali na kumshukuru Kaimu
Mkurugenzi Mkuu kwa kuwapa fursa ya kukutana naye, lakini alimuomba kuendelea
kudumisha mahusiano baina ya mwajiri na Tughe.
Pia alimuomba
aitake menejimenti yake kuwa na utaratibu wa kuweka milango wazi kwa
wafanyakazi kama yeye ili waweze kusikiliza na kutoa majibu sahihi kwa baadhi
ya masuala ya kiofisi yanayowasilishwa na wafanyakazi kwao na sio kila jambo
liwasilishwe kwake.
“Tunakuombea kwa
Mungu akutie nguvu kwa haya unayotaka kufanya likiwemo la kuboresha maslahi ya
wafanyakazi kwa kuwa litasaidia kuamsha morali ya kazi kwa wafanyakazi, lakini
hii sera yako ya kuwacha milango wazi, tunaomba nayo itekelezwe katika ngazi ya
menejimenti yako kwani kuna mambo ambayo yanaweza kumalizwa na Wakurugenzi na
Mameneja wenyewe na sio lazima yafike kwako, “ alisema Bw. Elias.
Katika kuboresha
maslahi ya wafanyakazi ambacho kimeonekana ni kipaumbele cha Kaimu Mkurugenzi
mkuu kwa wafanyakazi, Bw. Elias amemuomba kuangalia namna bora ya kusimamia
maslahi hayo ikiwemo kuuasili mkataba wa hali bora (SBA) kama inavyotekelezwa
na taasisi nyingine za serikali.
Subscribe to:
Comments (Atom)