Tuesday 6 September 2016

Kocha Mauritania hana uhakika na hatma yake licha ya timu kufanya vizuri michuano ya kufuzu kwa afcon 2017 gabon



NOUAKCHOTT, Mauritania
KOCHA wa Mauritania Corentin Martins (pichani) hana uhakika wa kuendelea kuwepo katika timu hiyo licha ya kuiongoza kumaliza vizuri hatua ya kufuzu ya Mataifa ya Afrika (Afcon 2017).

Sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya Afrika Kusini huko Nelspruit kuliihakikishia Mauritania kumaliza katika nafasi ya pili katika kundi lake.

Wamekosa nafasi ya kufuzu kwenda Gabon mwakani lakini Martins alisema kuwa kundi lao, ambapo pia likuwa na timu za Afrika Kusini na Gambia, lilikuwa moja ya makudni ya kifo.

Mchezaji huyo wazamani wa Ufaransa, ambaye timu yake ilikuwa na nafasi finyu kimahesabu ya kufuzu kwa fainali hizo kama ingeshinda mchezo huo, alisema alikuwa akitarajia kumaliza wa pili katika msimamo wa kundi lao.

"Kwan chi ambayo haija wachezaji wengi wenye uzoefu katika soka la kimataifa, tumepiga hatua kubwa, alisema kiungo huyo wazamani wa Auxerre.

"Zaidi ya miaka miwili, tulikuwa na nafasi kucheza na timu kutoka mataifa makubwa kisoka Afrika na kujifunza mengi kutoka kwa wazoefu. Ilikuwa nafasi finyu kwa Mauritania kupata nafasi kama ile ya kucheza na timu kubwa.

"Kufanya vizuri dhidi yao tulitupatia kujiamini sana. Mara mbili tumeshindwa kwa bao moja na Cameroon, na tulifungwa kidogo na Tunisia katika mchezo wa kufuzu kwa Kombe la Dunia na tulipata pointi nne kutoka kwa Afrika kusini. 
Nafikiri tunaweza kuendelea kupata matokeo mazuri.

Mauritania kwa muda mrefu ilikuwa ikichukuliwa kuwa ni taifa dogo katika soka lakini baada ya sare ya Ijumaa inatarajia kupanda viwango vya Fifa na kwa mara ya kwanza kufikia katika 100 katika kipindi cha miaka 20.

"Kwa kweli tulikuwa tukifanya kazi kwa bidii kuongezea ubora timu hii na ninafikiri tumesonga mbele kwa haraka sana, alisema Martins.

Lakini kocha huyo mwenye umri wa miaka 47, ambaye alinza kazi yake na Mauritania Oktoba miaka miwili iliyopita, alisema kuwa hajui kama atapewa ofa nyingine ya kuendelea kuifundisha timu hiyo.

Mkataba wake wasasa unatarajia kumalizika Desemba mwaka huu.

 "Nina furahia sana kazi hii, watu wa hapa ni wazuri sana kwangu na nimekuwa na uhusiano mzuri na uongozi. Bila shaka, sio kitu rahisi kuwa kocha wa timu ya taifa-unaathirika sana unapokuwa katika benchi.alitania kocha huyo. Lakini sijui kitu gani kitatokea sasa.

Mauritania ilipoteza mechi mbili tu kati ya sita za kundi lake la M, ambapo ilimaliza ikiwa na point inane.

Katika mashindano ya kufuzu yaliyopita ilimaliza ya mwisho kimsimamo, na haikuwahi kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika.

No comments:

Post a Comment