Tuesday 6 September 2016

Hispania yaichakaza kibonde Liechtenstein mabao 8-0, Italia ikishinda 3-1 mbio za kwenda Urusi 2018



Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya Hispania wakishangilia moja ya mabao yao dhidi ya  Liechtenstein.
MADRID, Hispania
HISPANIA imetoa onyo kwa timu zinazoshiriki katika kinyanganyiro chakusaka tiketi ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya Liechtenstein.

Mabao yao saba yalipatikana katika kipindi cha pili wakati Liechtenstein wakijaribu kupambana baada ya kuwapelekesha wenyeji wao mwanzoni mwa mchezo.

Diego Costa, David Silva na Alvaro Morata wote kila mmoja alifunga mara mbili wakati Sergi Roberto na Vitolo nao pia waliingia katika orodha ya wafungaji katika mchezo huo wa ufunguzi wa Kundi G.

Huo n mwanzo mzuri katika mchezo wa kwanza wa kimashindano kwa kocha Julen Lopetegui, ambaye alihusika kwa timu yake kupata ushindi kiduchu baada ya kuwa mbele kwa bao 1-0 hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.

Matokeo hayo yaliwafanya kuwa vinara wa awali wa Kundi G lakini Italia nayo ilianza kwa ushindi wa 3-1 licha ya kujkuta ikipunguzwa na kubaki na wachezaji 10 walipocheza dhidi ya Israel katika mchezo uliofanyika Haifa.

Graziano Pelle alikiwezesha kikosi cha kocha Giampiero Ventura kuanza vizuri kampeni zake kabla Antonio Candreva hajaongeza bao jingine alilofunga kwa penalti na kuihakikishia ushindi timu hiyo.

Tal Ben Chaim aliifungia Israel bao la kufutia machozi lakini Ciro Immobile aliongeza na kuifanya Italia kukamilisha ushindi wake wa mabao 3-1 licha ya kutolewa kwa mchezaji wake Giorgio Chiellini.

Mchezo mwingie wa kundi hilo haukumalizika wakati Albania ikicheza na wajirani zao wa Macedonia huko Shkoder ilibidi kusimamishwa baada ya dakika 77 kufuatia mvua kubwa kunyesha.

Wakati mchezo huo unasimama timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1 kwa bao la Ergjan Alioski ambalo lilikuwa linajibu lile la Armando Sadiku alilofunga mapema.

Kosovo nao ilianza vizuri kucheza mashindano hayo ya kufuzu kwa Kombe la Dunia baada ya kutoka nyuma na kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo wao wa kwanza wa kufuzu katika mchezo uliofanyika Finland.l

Mchezaji wazamani wa Norway Valon Berisha mmoja kati ya wachezaji sita walihalalishwa kucheza saa chache kabla ya kuanza kwa mchezo huo, alifunga bao la kusawazisha kwa penalti baada ya dakika 60.

Paulus Arajuuri aliipatia Finland bao la kuongoza katika mchezo wa Kundi I, lakini Kosovo, ikicheza mchezo wake wa kwanza wa mashindano ya kimataifa, ilicheza vizuri na walipiga mwamba kupitia kwa Leart Paqarada kabla Berisha hajaiwezesha timu hiyo kuondoka na pointi.

Hiyo ni moja kati ya sare tatu za 1-1 katika kundi hilo, huku zingie zikiwa ni kati ya Croatia na Uturuki huko Zagreb na Ukraine na Iceland huko Kiev ambazo nazo zilimalizika kwa sare kama hiyo.

Katika Kundi D, mbaop kutoka kwa Martin Hinteregger na Marc Janko yaliisaidia Austria kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Georgia huko Tbilisi.Bao la kufutia machozi lilifungwa na Jano Ananidze.

Kwingineko katika Kundi D, Ireland ilitoka sare ya kufungana mabao 2-2 na Serbia huku Wales ikiichapa Moldova 4-0.

No comments:

Post a Comment