Sunday 11 September 2016

Angelique Kerber adhihirisha makali yake kwa kutwaa taji la US Open 2016 kwa kumfunga Karolina Pliskoya



 
NEW YORK, Marekani
MJERUMANI Angelique Kerber (pichani), aliendeleza makali yake kama bingwa namba moja kwa ubora duniani baada ya jana kuchapa Mczech Karolina Pliskova katika mchezo wa fainali ya mashindano ya US Open.

Kerber, 28, alishinda kwa 6-3 4-6 6-4 katika mchezo huo uliofanyika jijini hapa akiongezea taji la US Open katika taji lake la Australian Open alilolitwaa Januari.

Ushindi wa Pliskova katika nusu fainali dhidi ya Serena Williams tayari uimhakikishia Mjerumani huyo namba moja katika viwango vipya vya ubou zote zimekuwa kweli leo (jana) na ninachojaribu sasa ni kufurahia mafanikio yangu sasa, alisema Kerber.

Kerber hiyo ilikuwa ni fainali yake ya tatu ya mashindano makubwa mwaka huu, ambapo Mjerumani huyo alicheza huku akisubiri kutangazwa bingwa namba moja duniani katika viwango vya mchezo huo.

No comments:

Post a Comment