Tuesday 16 October 2018

Taa Yakabidhi Mafuta ya Ngozi kwa Wanafunzi Wenye Ualibino

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Naomi Semadio (kulia) akiteta na Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Jeshi la Wokovu, Masoud Babu wakati TAA ilipokabidhi mafuta kwa wwanafunzi walemavu wa ngozi leo Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege imetoa msaada wa mafuta kwa wanafunzi walemavu wa ngozi wa shule za msingi za Uhuru Mchanganyiko na ile ya Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam.

Jumla ya chupa 55 za mafuta hayo ya ngozi aina ya Infinity Care SPF 30 Sun Screen, ambapo kichupa kimoja kina gharama ya Sh 25,000 na kufanya gharama yote kuwa ni Sh 1,375,000.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tazania (TAA), Naomi Semadio akimkabidhi mafuta mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni mwalimu wa shule ya Msingi ya Jeshi la Wokovu, Masoud Babu na kushoto ni Katibu Mkuu wa Taifa Chama cha Wenye Ualibino Tanzania, Mussa Kabimbi.
Akikabidhi mafuta hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela, mwakilishi huyo Naomi Semadio alimkabidhi kila mwanafunzi kichupa cha mafuta hayo kwa ajili ya matumizi ya kila siku.

Alisema kuwa hatua hiyo ya TAA ya kutoa msaada huo ni sehemu ya kawaida ya sera ya mamlaka hiyo kusaidia jamii kwa kutatua matatizo yake, ambapo kwa vijana hao, changamoto kubwa kwao ni matatizo ya ngozi.
Alisema wamekuwa wakitoa misaada kwa jamii bila kuwepo kwa ubaguzi wa aina yoyote, ambapo hivi karibuni imefanikisha tamasha la urithi wetu lililofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam pamoja na kusaidia Umoja wa Wabunge Wanawake kwa ajili ya kujenga vyoo.

Mwalimu wa shule ya Msingi Jeshi la Wokovu Masoud Babu aliipongeza TAA kwa msaada huo na kusema kuwa wanafunzi wao albino wamekuwa na changamoto nyingi ikiwemo hiyo ya tatizo la afya, na hasa ngozi.
Alisema asilimia 70 ya watu wenye alboni wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na saratani ya ngozi, pia alitaka kofia na miwani kwa ajili ya kuwakinga wanafunzo hayo.
Alisema gharama ya kumtibu mtoto albino ni kubwa na amewapogeza TAA na kuutumia vizuru msaada huo na amewataka wasiwasahau, waendelee kuwasaidia.

“Msaada huu utakuwa ni mwanzo kwani wanatarajia TAA itaendelea kuwasaidia kwa masuala mbalimbali, hasa ukizingatia mafuta hayo yana gharama kubwa na wengi wanashindwa kumudu gharama zake, “alisema mwalimu huyo.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Jeshi la Wokovu, Rehema Mwahalende alishukuru TAA kwa msaada huo kwani utawasaidia wanafunzi hao kuepukana na matatizo ya ngozi, ambayo yanasababisha saratani.
Alisema TAA imeonesha mfano wa kuigwa kwa kuwajali watoto hao na wanatarajia wataendelea kuwasaidia katika nyanja mbalimbali.
Mkurugenzi Msaidizi wa Jeshi la Wokovu Mgulani Jijini Dar es Salaam, Meja Rehema Mwahalende akizungumza baada ya TAA kukabidhi mafuta ya ngozi kwa wanafunzi wa shule hiyo na ile ya Uhuru Mchanganyiko leo Mgulani Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment