Friday 19 October 2018

Makocha Judo Wapatiwa Mafunzo Yaufundishaji

Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akizungua mafunzo ya makocha wa judo yanayoendelea Mkuza, Kibaha mkoani Pwani.

Na Mwandishi Wetu, Pwani
WALIMU 30 wa mchezo wa Judo kutoka mikoa mbalimbali wanashiriki mafunzo ya ukocha 'Level III' yaliyoanza jana kituo cha michezo cha Filbert Bayi, Mkuza Kibaha mkoani Pwani.

Mafunzo hayo yaliyofunguliwa juzi, yameandaliwa na Chama cha Judo Tanzania (JATA), Chama cha Judo Zanzibar (ZJA), na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), chini ya ufadhili wa Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC), kupitia kitengo chake cha Olimpic Solidarity (OS).
Wakufunzi wa mafunzo ya mchezo wa judo wakifuatilia ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuza, Kibaha.
Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa mafunzo hayo Mkuza Kibaha juzi, yanayofundishwa na mkufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Judo (IJF), Meridja Omar wa Algeria, Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi alisema mafunzo hayo ya makocha ni ya level 111.

Bayi alisema kuwa mafunzo hayo ni kati ya mawili ambayo yako kwenye Kalenda ya shughuli za Kamati ya Olimpiki Tanzania mwaka 2018, ambapo mengine kama hayo yalikuwa ya mchezo wa Mpira wa Meza, ambayo yalifanyika wiki chache zilizopitakwa ufadhili wa OS.
Washiriki wa mafunzo ya ufundishaji mchezo wa judo wakiwa katika picha ya pamoja na mkufunzo wao, meridja Omar (wa sita kutoka kulia mstari wa mbele), Mkuza, Kibaha mkoani Pwani. 
Alisema awali TOC waliomba OS kwa kukifahamisha Chama cha Judo Tanzania kuandaa mafunzo ya walimu wa mchezo wa Judo kwa daraja la I (II), ili kupata walimu wengi wa madaraja hayo watakaoweza kueneza zaidi mchezo huo katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.

"Vyama vya mchezo wa Judo Bara na Zanzibar kwa kufahamu au kutofahamu, wakawasilisha TOC baadhi ya majina wa walimu waliohudhuria mafunzo ya Daraja la I/II yaliyofanyika mwaka 2011... Naipongeza ofisi yangu ya TOC kwa kugundua hilo na kulishughulikia suala hili la kurekebisha daraja kwa kushirikiana na IJF, “alisema Bayi.

Katibu Mkuu wa Chama cha Judo Tanzania (Taja), Innocent Mallya (kushoto) na mratibu wa mafunzo hayo kutoka Kamati ya Olimpiki Tanzania, TOC, Ame.
TOC imekuwa ikijitahidi kusaidia vyama na mashirikisho ya michezo mbalimbali nchini hasa kwa mafunzo ya walimu, utawala, wanawake na michezo, lakini bado baadhi hawatambui au kama wanatambua basi hawatumii nafasi hizi vizuri.

Alisema TOC ipo tayari kutoa  elimu kwa walimu wa vyama vya michezo, ambao watakuwa na uhitaji pale wakati wao utakapofika.
"Nia na malengo ya Kamati ya Olimpiki ni vyama vya michezo kuwa na walimu wengi, watakaokuwa na taaluma ya kuwandaa wanamichezo watakaokuwa washiriki wazuri kutuwakilisha katika mashindano ya kimataifa na kutuletea medali," alisema.

Aliongeza kuwa, Tanzania ina vipaji vingi vya mchezo wa Judo, kinachokosekana ni walimu wenye ufahamu unaotakiwa katika ngazi za kimataifa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jata, Innocent Mallya, mbali na kushukuru kwa kupata mafunzo hayo, aliwataka washiriki kuzingatia mafunzo na kwenda kuutumia ujuzi huo katika kuzalisha wachezaji wapya huko watokako.
Mkufunzi wa Kimataifa wa Mafunzo ya Makocha wa mchezo wa judo, Meridja Omar kutoka Algeria. 
Mallya, alisema hivi sasa malengo ni kwa vijana kwani katika klabu nyingi hapa nchini wachezaji wengi walioko hawana muda mrefu kuendelea kucheza, hivyo ni jukumu la makocha hao kwenda kuibua vipaji vipya.

Washiriki mbalimbali wa mafunzo hayo walisema kwa nyakati tofauti, mafunzo hayo yatawasaidia kuibua vipaji vipya katika mchezo huo, hasa katika shule mbalimbali nchini.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa makocha wa judo mjini Kibaha, akijitambulisha.
Mafunzo hayo ambayo yatasaidia sana kuuendeleza mchezo huo kwa kuibua vipaji vipya, yanatarajia kukamilika Oktoba 24 mwaka huu, ambako washiriki watakabidhiwa vyeti baada ya kufanya mitihani yao.
Katibu Mkuu wa Chama cha Judo Tanzania (Taja), Inndo Mkuza Kibaha mkoani Pwani.ocent Mallya akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa makocha wa mchezo wa judo.


No comments:

Post a Comment